Taarifa zinasema kuwa, katika nchi nyingine kama vile Umoja wa Falme za Kiarabu, Jordan, Kuwait, Yemen, Syria, Lebanon, Afghanistan, Tajikistan, Kazakhstan na Palestina leo Jumatatu ni tarehe Mosi Shawwal. Hali kadhalika, baadhi ya Waislamu nchini Rwanda na Kenya leo wanasherehekea sikukuu ya Idul Fitr.
Hata hivyo, nchi nyingi duniani zimetangaza kuwa kesho Jumanne ni tarehe Mosi Shawwal. Nchi kama vile Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Algeria, Pakistan, Tanzania na Azerbaijan zimetangaza kuwa sherehe za Idul Fitr zitaanza kesho Jumanne.
1433605