IQNA

Kikao cha OIC kuhusu vijana na vyombo vya habari katika Uislamu

13:02 - April 30, 2015
Habari ID: 3233866
Kikao cha kumi cha kamati ya kudumu inayohusika na masuala ya utamaduni na habari ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kuhusu nafasi ya vijana na vyombo vya habari katika kudumisha amani na uthabiti katika Ulimwengu wa Kiislamu kimefanyika Dakar, mji mkuu wa Senegal.

Kikao hicho kilifunguliwa Jumanne kwa hotuba ya kwa kuhudhuriwa na Rais Macky Sall wa nchi hiyo. Iyad Madani, Katibu Mkuu Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu,  Mkuu wa Kamati ya Kudumu ya Masuala ya Utamaduni na Habari wa OIC na vile vile Mawaziri wa Utamaduni na Habari wa nchi za Kiislamu pia wamehudhuria  na kuhutubi katika kikao hicho cha Dakar.

Semina hiyo ya siku mbili ilitupia jicho masuala mengi kama mazungumzo kati ya tamaduni na staarabu mbalimbali na pia nafasi ya vyombo vya habari vya Ulimwengu wa Kiislamu katika kuiunga mkono Quds Tukufu na kadhia ya Palestina.../EM

3228651

captcha