IQNA

Wananchi wa Iran waandamana kulaani jinai za Saudia nchini Yemen

19:27 - May 09, 2015
Habari ID: 3276822
Mamilioni ya wananchi Waislamu wa Iran wameandamana kote nchini baada ya Sala ya Ijumaa kulaani jinai za utawala wa Saudia dhidi ya watu wa Yemen. Wananchi katika miji mikubwa kama vile Tehran, Qom, Mashhad na miji mingine 770 kote nchini.

Wameandamana wamelaani vikali mauaji ya umati ya Waislamu wasio na ulinzi wala hatia wa Yemen ambao wamepoteza maisha katika hujuma zinazoongozwa na utawala dhalimu wa Saudi Arabia. Aidha waandamanaji hao wametaka jinai hizo za Saudia zisitishwe mara moja. Huku wakitoa nara kama vile 'Mauti kwa Marekani', 'Mauti kwa Aal Saud' na 'Mauti kwa Utawala wa Kizayuni' waandamanaji wametangaza uungaji mkono wao kwa  wananchi wasio na hatia Yemen. Baada ya maandamano hayo kumesomwa taarifa ya kulaani hujuma ya Saudia Yemen na njama za Marekani za kuhakikisha utawala wa Kizayuni unabakia katika eneo. Taarifa hiyo imesema Riyadh, mji mkuu wa Saudia sasa ni mji mkuu wa ugaidi. Halikadhalika wamelaani mpango wa pamoja wa Saudi Arabia na Wazayuni katika kuizingira Yemen na kuzuia misaada ya kibinadamu kuingizwa nchini humo. Wakati huo huo Mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika Hilali Nyekundu ya Iran ameashiria hatua ya Saudia kuzuia misaada ya kibinaadmau kutoka Iran isiwafikie wanaohitajia nchini Yemen. Hujatul Islam wal Muslimin Muizz amesema kuwa, meli ya misaada ya kibinadamu kutoka Iran kesho itaelekea Yemen.../mh

3273280

Kishikizo: iran yemen saudi jinai
captcha