IQNA

Majaji wa mashindano ya Qur’ani Iran wateuliwa

18:09 - May 12, 2015
Habari ID: 3293178
Wataalamu 22 wa Qur’ani Tukufu wameteuliwa katika jopo la majaji wa awamu ya 32 ya Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Katibu wa mashindano hayo Seyed Mustafa Husseni amesema majaji 12 watakuwa ni kutoka Iran huku wengine 10 wakiwa ni kutoka mataifa mbali mbali duniani.
Ahmed Khalid al-Athamina kutoka Jordan, Seyed Aqil Hussein al-Munawar kutoka Indonesia, Nureddin Mohamedi kutoka Algeria, na Khalil al-Nour bin Muhammad kutoka Malaysia ni kati ya majaji wa kigeni katika mashindano, amesema. Kwa mujibu wa Husseini, mtaalamu maarufu wa Qur’ani kutoka Iran, Sheikh Abdul Rasul Aba indie atakayekuwa mwenyekiti wa jopo hilo.
Awamu ya 32 ya Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yanatazamiwa kuanza katika mji mkuu Tehran mnamo 27 Rajab sawa na Mei 15.
Mashindano hayo yataanza sanjari na mnasaba wa Mab’ath (kubaathiwa  au kupewa utume Mtume Muhammad SAW).  Mashindano hayo ya kila mwaka yataendelea kwa muda wa wiki moja hadi Ijumaa tarehe 22 Mei.

3290825

captcha