IQNA

Washindi wa Mashindano ya Qur’anI ya Mkoa wa Tehran waenziwa

14:45 - August 01, 2025
Habari ID: 3481028
IQNA – Washindi wa upande wa wanaume katika awamu ya kimkoa ya Mashindano ya 48 ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu nchini Iran, yaliyofanyika Tehran, wametangazwa rasmi katika hafla ya kufunga mashindano hayo na kukabidhiwa vyeti vya heshima pamoja na zawadi za fedha.

Hafla hiyo ilifanyika jioni ya Jumanne katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Eram, ikihudhuriwa na mashekhe, wataalamu wa masuala ya Qur’ani, na viongozi wa dini, akiwemo Mkuu wa Taasisi ya Awqaf na Mambo ya Hisani, Hujjatul-Islam Sayyid Mehdi Khamoushi.

Majina ya washindi waliotangazwa kuwa wa juu katika nyanja mbalimbali ni:
Mohammad Reza Jafarpour, Mohammad Javad Assadi Majd, Ahmad Barzegar, Mohammad Mehdi Hajizdeh, Reza Shaabani, Rasoul Bakhshi, Hamid Reza Nasirifar, Amir Hossein Landarani, na Ehsan Rahmani.

Mashindano haya yalianza Ijumaa, Julai 25, katika Hoteli ya Eram kwa makundi mawili: wanaume na wanawake. Katika raundi hii, kulikuwa na washiriki 118 wa upande wa wanawake na 179 wa upande wa wanaume waliokuwa wakishindana katika nyanja zifuatazo:

  • Kisomo cha Qur’an kwa tajwid (qira’a), Kisomo kwa tarteel, Kuhifadhi Qur’an yote, Kuhifadhi Juz’u 20, Kuhifadhi Juz’u 10, Adhana (kwa wanaume pekee), na Kisomo cha dua (munajat).

Washindi wa awamu hii ya kimkoa wataendelea kushiriki katika awamu ya kitaifa ambayo imepangwa kufanyika kwa sehemu mbili: awamu ya mchujo na awamu ya fainali.

Mkoa wa Kurdistan (magharibi mwa Iran) umepangwa kuwa mwenyeji wa hatua ya mwisho ya mashindano hayo.

3494060/

captcha