Dkt. Tarouti ambaye alikuwa jaji katika Mashindano ya 57 ya Kimatiafa ya Qur’ani Malaysia mwezi Juni, ambapo qarii Muirani aliyeaga dunia Mina Mohsen Hajihassani Kargar alichukua nafasi ya kwanza, katika ujumbe maalumu uliopokewa na IQNA amesema amepata huzni na majonzi kufuatia kifo cha qarii huyo Muirani.
Katika ujumbe wake Ustadh Tartouti amesema: "Nimeumia moyo kwa kuwa, wakati nimetimiza faradhi ya Hija na nilipokuwa nikirejea nyumbani nilipokea habari kuwa Mohsen Hajihassani Kargar ameitikia mwito wa Mola wake kwa kutamka Labbayk na kurejea mbele ya haki. Nilikuwa takribani mita 300 kutoka eneo la tukio na wala sikudhani Mohsen, azizi wangu, alikuwa miongoni mwa mashahidi. Kwa baraka ya Qur'ani anaelekea peponi."
Akizihutubu familia za maqarii wa Qur'ani waliokufa shahidi Mina, Ustadh Tarouti amesema: "Hampaswi kuomboleza bali kwa hakika mnastahiki pongezi kwa fadhila na karama za Allah SWT. Hii ni kwa sababu mashahidi wenu wa Qur'ani wameitikia mwito wa Allah SWT na kutamka Labbayk naye Allah SWT akawachukua waja wake hao wakiwa katika hali ya kuwa wamevalia vazi la Ihramu."
Ikumbukwe kuwa Alhamisi iliyopita mahujaji takribani 2,000 wakiwemo Wairani 136 wamethibitishwa kupoteza maisha katika maafa ya Mina. Miongoni mwa waliopoteza maisha walikuwemo maqarii wawili wa kimataifa wa Iran, Mohsen Hajihassani Kargar na Amin Bavi.../mh