IQNA

Maqarii wa Kishia washiriki kikao cha Qur'ani Saihat, Saudia

0:07 - January 26, 2016
Habari ID: 3470088
Kikao cha 11 cha kila mwaka cha kusoma Qur'ani Tukufu kimefanyika katika Msikiti wa Ummul Banyn katika mji wa Saihat mashariki mwa Saudi Arabia.
Kwa mujibu wa gazeti la Juhaina al Ekhbariya, Kikao hicho cha 11 cha kila mwaka cha kusoma Qur'ani Tukufu kimehudhuriwa na shakhsia 400 wa kidini na kijamii, maqarii kutoka Saudi Arabia na nchi jirani za Ghuba ya Uajemi. Kikao hicho cha kujikurubisha na Qur'ani Tukufu kimefanyika katika Msikiti wa Jamia ya Ummul Banin katika mji wa Saihat wenye wakaazi wengi Waislamu wa madhehebu ya Shia.
Kikao hicho cha kimataifa ya Qur'ani Tukufu kimefanyika kwa himaya ya  Taasisi ya Anwar al Qur'an katika mji huo ulio katika mkoa wa Qatif nchi Saudia.
Kikao hicho cha kujikurubisha na Qur'ani Tukufu kilijumuisha maqarri maarufu  wakiwemo Mohammad Al Busaidi na Hussein Aal Rabaan kutoka Taasisi ya Anwar al Qur'an ya mjini Saihat, Hashim al Shaalah, Said Abdulkarim Aal Issa, na Saeed Sharufna ambao ni maqarri kutoka mkoa wa Qatif, Mohammad Yassin Jubayl ambaye ni qarii kijana wa Kishia kutoka Bahrain, Ahmad al Muhaysini ambaye ni kati ya Mashia wa mjini Madina na Haj Hassan Aal Qanbar mmoja kati ya maqarii wa Kuwait.
Lengo la kuandaliwa kikao hicho cha kujikurubisha na Qur'ani Tukufu limetajwa kuwa kuimarisha na kueneza mazingira ya Qur'ani katika jamii, kuwaarifisha maqarii bora na kuimarisha uhusiano baina ya taasisi za Qur'ani kwa lengo la kustawisha harakati za Qur'ani.
Abdul Jabbir al Shafii Mkuu wa Taasisi ya Qur'ani ya Anwar al Qur'an alihutubu katika kikao hicho na kusema: "Taasisi hii inajitahidi kuandaa program ili watu waweze kuvutiwa na mafundisho ya Qur'ani na pia kuwalea vijana na mabarobaro kwa msingi wa  Qur'ani,  thamani za kidini na maadili bora.
3469918
captcha