IQNA

Taarifa ya Jeshi la Iran kuhusu Siku ya Kimataifa ya Quds

17:41 - June 28, 2016
Habari ID: 3470419
Kamandi ya Majeshi yote ya Iran imetoa wito kwa wote katika ulimwengu wa Kiislamu kujitokeza kwa wingi katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds Ijumaa hii.
Katika taarifa kwa munasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds, Kamandi ya Majeshi yote ya Iran imesema, ubunifu wa kistratijia wa Imam Khomeini MA, katika kuitangaza Ijumaa ya mwisho ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuwa Siku ya Kimataifa ya Qudsn ni fursa kwa ajili ya mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel ambao ungali changamoto kubwa katika umma wa Kiislamu.
Wakati huo huo, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, Ali Larijani amesema: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaunga mkono kikamilifu taifa la Palestina katika mapambano yake dhidi ya utawala wa Kizayuni."
Larijani ameyasema hayo Jumanne mjini Tehran wakati alipokutana na wanaharakati kadhaa wanaohusika na mapmabano ya kuikomboa Quds Tukufu na Palestina kutoka minyororo ya Wazayuni. Larijani amesema kuunga mkono Palestina ni katika stratijia muhimu za Iran. Larijani amesema Siku ya Kimataifa ya Quds ni nembo ya azma na irada ya mataifa katika kupigania ukombozi wa Palestina.
Ijumaa Julai Mosi ni Siku ya Kimataifa ya Quds ambapo watu kutoka matabaka mbali mbali duniani wanatazamiwa kuandamana na kujumuika kwa lengo la kufungamana na mapambano ya ukombozi wa Palestina sambamba na kuulani utawala wa Kizayuni wa Israel na waitifaki wake.
3511039
captcha