
Katika taarifa kwa munasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds,  Kamandi ya 
Majeshi yote ya Iran  imesema, ubunifu wa kistratijia wa Imam Khomeini 
MA, katika kuitangaza Ijumaa ya mwisho ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani 
kuwa Siku ya Kimataifa ya Qudsn ni fursa kwa ajili ya mapambano dhidi ya
 utawala wa Kizayuni wa Israel ambao ungali changamoto kubwa katika umma
 wa Kiislamu.
Wakati huo huo, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, 
Ali Larijani amesema: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaunga mkono 
kikamilifu taifa la Palestina katika mapambano yake dhidi ya utawala wa 
Kizayuni." 
Larijani ameyasema hayo Jumanne mjini Tehran wakati alipokutana na 
wanaharakati kadhaa wanaohusika na mapmabano ya kuikomboa Quds Tukufu na
 Palestina kutoka minyororo ya Wazayuni. Larijani amesema kuunga mkono 
Palestina ni katika stratijia muhimu za Iran. Larijani amesema Siku ya 
Kimataifa ya Quds ni nembo ya azma na irada ya mataifa katika kupigania 
ukombozi wa Palestina.
Ijumaa Julai Mosi ni Siku ya Kimataifa ya Quds ambapo watu kutoka 
matabaka mbali mbali duniani wanatazamiwa kuandamana na kujumuika kwa 
lengo la kufungamana na mapambano ya ukombozi wa Palestina sambamba na 
kuulani utawala wa Kizayuni wa Israel na waitifaki wake.
3511039