IQNA

Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Lebanon yamalizika

22:33 - July 16, 2021
Habari ID: 3474106
TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Qur’ani ya Tawjih na Irshad ya Lebanon imetangaza washiriki 10 bora wa Mashindano ya Kwanza ya Kimataifa ya Qur’ani ya Oula-al-Qiblatain.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA,  nafasi ya kwanza katika mashindano hayo ya qiraa ya Qur’ani Tukufu imechukuliwa na Abdullah Karbalai wa Iraq ambaye amefuatiwa na Mohammad Ali Qassim wa Lebanon huku nafasi ya tatu akiwa ameshika Majid Ananpour wa Iran.

Jumuiya ya Qur’ani ya Irshad wa Tawjih ya Lebanon inapata himaya ya Sayyid Hassan Nasrallah, Katibu Mkuu wa Hizbullah na imeandaa mashindano hayo ya Qur’ani kwa njia ya intaneti.

Mashindano hayo yalianza Jumamosi 10 Julai na washindi wammetangazwa leo Ijumaa.

Wasomaji  Qur’ani 322 kutoka nchi 40 duniani wameshiriki katika duru za mchujo za mashindano hayo na hatimaye washiriki 10 bora wametangazwa.

/3984414

captcha