IQNA

Waalimu 114 wanaofunza kuhifadhi Qur'ani Iran kuenziwa

10:23 - December 12, 2021
Habari ID: 3474667
TEHRAN (IQNA)- Waalimu 114 wa ngazi za juu wanaofunza kuhifadhi Qur'ani nchini Iran wataenziwa katika mashindano yajayo ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran.

Kwa mujibu wa taarifa kamati maalumu imeundwa kuwachagua waalimu bora zaidi wa taaluma ya kuhifadhi Qur'ani nchini Iran.

Wawakilishi wa Wizara ya Utamaduni na Muongozi wa Kiislamu, Kanali ya Qur'ani ya IRIB, Taasisi ya Darul Qur'an Karim na taasisi zingine kadhaa wanaunda kamati hiyo ambayo itakuwa na matawi katika miko yote ya Iran.

Imedokezwa kuwa kati ya vigezo vya kuchaguliwa waalimu hao ni kwa kwa uchaguze wawe wamehifadhi Juzuu 10 za Qur'ani na wawe na uzoefu wa miaka mitano katika ufundishaji kuhifadhi Qur'ani Tukufu.

Mashindano ya 38 ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani ya Iran yanatazamiwa kufanyika Machi 2022 mjini Tehran.

4020104

captcha