IQNA

Wawakilishi wa Iran katika mashindano ya kimataifa ya Qur’ani ya wanafunzi wabainika

23:57 - November 24, 2021
Habari ID: 3474595
TEHRAN (IQNA)- Iran imetangaza kubuni timu ya makundi manne kushiriki katika mashindano yajayo ya kimataifa ya Qurani ya wanafunzi.

Akizungumza na IQNA Jumatano, Mikail Baqeri, mkurugenzi mkuu wa Qur’ani Etrat na Sala katika Wizara ya Elimu ya Iran amesema timu ya  iran inajumuisha timbu mbili za wavulana na wasichana ambazo zitashiriki katika kategoria za kuhifadhi na kusoma Qur’ani.

Mchujo wa kuchagua wawakilishi wa Iran ulianza mwezi moja uliopita na majaji  wamekuwa wakiwasikiliza washiriki kwa njia ya intaneti.

Mashindano hayo ya kimatiafa ya Qur’ani ya wanafunzi wa shule hufanyika mara moja kila miaka miwili nchini Iran. Mashindano ya awamu hii yanatazamiwa kufanyika baina ya Februari na Machi 2022 sambamba na mashindano ya kimataifa ya Qur’ani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Baqeri anasema mazingira yakiruhusu, fainali ya mashindano hayo itafanyika hapa mjini Tehran kwa kushiriki ana kwa ana washindani.

4015904

captcha