IQNA

Hija 1435

Msafara wa Nur wa Iran waandaa vikao vya qiraa ya Qur’ani mjini  Madina

18:54 - May 31, 2024
Habari ID: 3478906
IQNA - Duru ya tano ya kikao cha qiraa ya Qur'ani Tukufu iliyohudhuriwa na wajumbe wa Msafara wa Nur wa Qur'ani kutokaIran, imefanyika katika mji mtakatifu wa Madina.

Duru hiyo Iliandaliwa katika Kituo cha Hayat al-Huda jijini Madina Jumatano usiku.

Maqari  mashuhuri Mehdi Adeli na Masoud Movahedirad walisoma Qur’ani Tukufu katika  hafla hiyo.

Adeli alisoma Aya za 64-69 za Surah An-Nisa na Movahedirad akasoma Aya za 101-108 za Surah Al-Anbiya.

Programu hiyo pia ilijumuisha qasida ya la Kundi la Al-Ibad.

Kila mwaka Waislamu zaidi ya milioni kutoka duniani kote hukusanyika Makka  kwa ajili ya Hija katika mwezi wa Dhul Hijja.

Iran pia hutuma mahujaji pamoja na kundi la wasomaji Qur'ani ambalo ni maarufu kama Msafara wa Nur wa Qur’ani Tukufu.

Wajumbe wa msafara huo huwa na vikao vya kusoma  Qur'ani nyakati mbali mbali  katika miji mitakatifu ya Makka na Madina.

 

4219222

captcha