IQNA

Ofisi ya Ayatullah Sistani yatoa taarifa kuhusu kuanza kwa Mwezi wa Ramadhani 

15:21 - February 20, 2025
Habari ID: 3480244
IQNA - Ofisi ya kiongozi mkuu au Marjaa Taqlid wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Ali al-Sistani, imetoa taarifa kuhusu kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka huu. 

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, inatarajiwa kwamba mwezi mwandamo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani utaonekana jioni ya Jumamosi, Machi 1

Hivyo basi, ofisi hiyo imetabiri kwamba Jumapili, Machi 2, 2025, itakuwa siku ya kwanza ya Mwezi wa Ramadhani

Ofisi ya Ayatullah Sistani katika mji mtakatifu wa Najaf pia imetabiri kwamba mwezi mwandamo wa mwezi wa Shawwal Hijri utaonekana jioni ya Jumapili, Machi 30

Hii inamaanisha kwamba Ramadhani ya mwaka huu itakuwa na siku 29 na Idul-Fitr, ambayo inaashiria mwisho wa Ramadhani, itakuwa Jumatatu, Machi 31

Ramadhani ni mwezi wa tisa na mtukufu zaidi katika kalenda ya Kiislamu, ambamo Waislamu wanakumbuka ufunuo wa Quran kwa Mtume Muhammad (SAW)

Wakati wa Ramadhani, Waislamu hufunga kutoka alfajiri hadi jioni, wakiepuka kula, kunywa, kuvuta sigara, na mahusiano ya ndoa

Pia hutumia muda zaidi kwa ibada mbali mbali, kutoa sadaka, na matendo mema, wakitafuta kuimarisha imani yao na kutakasa roho zao

Baadhi ya wasomi wa Kiislamu hutegemea mahesabu ya kinujumu au kianga ili kubaini mwanzo wa miezi ya mwandamo, wakati wengine wengi wanaamini kuwa kutazama mwezi kwa macho moja kwa moja au kutumia vifaa kama vile teleskopu ndiyo njia inayopaswa kutumika katika kubaini mwanzo na mwisho wa Mwezi wa Ramadhani.

3491926

Habari zinazohusiana
captcha