IQNA

Ayatullah Sistani atangaza Jumapili Kuwa Siku ya Kwanza ya Ramadhani

21:01 - March 01, 2025
Habari ID: 3480281
IQNA – Ofisi ya kiongozi mkuu wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Ali al-Sistani, imetangaza Jumapili, Machi 2, kuwa siku ya kwanza ya Ramadhani katika nchi hiyo ya Kiarabu.

Ofisi hiyo ilisema kwamba kuonekana mwezi mwandamoi hakuthibitishwa kwa Ayatullah Sistani jioni ya Ijumaa, hivyo Jumamosi imekuwa siku ya mwisho ya mwezi wa Hijri wa Shaaban nchini Iraq na maeneo jirani.

Kwa hiyo,  Ramadhani ya 1446 Hijri itaanza siku inayofuata, Jumapili, Machi 2.

Waislamu katika nchi kadhaa zingine, ikiwa ni pamoja na Iran, pia wataanza mwezi wa kufunga Jumapili.

Wakati huo huo, nchini Saudi Arabia, Misri, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu, Bahrain, Kuwait, Lebanon, Palestina, Morocco, Tunisia, Mauritania, Indonesia, na Malaysia, Jumamosi ndiyo siku ya kwanza ya Ramadhani.

Ramadhani ni mwezi wa tisa na mtakatifu zaidi katika kalenda ya Kiislamu, ambapo Waislamu hukumbuka Wahyi  wa Qur’ani kwa Mtume Muhammad (SAW).

Wakati wa Ramadhani, Waislamu hufunga kutoka alfajiri hadi magharibi, wakijizuia kula, kunywa, na kuvuta sigara. Pia hutumia muda zaidi kwa sala, sadaka na matendo mema, wakitafuta kuimarisha imani zao na kutakasa roho zao.

Baadhi ya wanazuoni wa dini hutegemea hesabu za kiastronomia ili kubainisha mwanzo wa miezi ya mwezi, wakati wengi wao wanaamini kwamba kuonekana kwa macho kwa mwezi mchanga ndiyo inapaswa kutumika katika kesi hii.

3492082

Habari zinazohusiana
captcha