Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika tovuti ya IAC mwezi mwandamo utaonekana Aprili 12 na hivyo siku itakayofuata itakuwa mwanzo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Nchi za Kiislamu ambazo kwa mujibu wa utabiri zitaweza kuuona mwezi mwandamo mnamo Aprili 12 bila tatizo ni pamoja na Algeria, Morocco, Mauritania, Iran, Indonesia, Malaysia, Oman, Umoja wa Falme za Kiarabu, Saudi Arabia na Syria.
Naye Ibrahim al Jarwan, mwanachama wa Jumuiya ya Waarabu ya Nujumu na Sayansi za Anga za Mbali (AUASS) naye pia ametabiri kuwa aghalabu ya nchi zinatazamiwa kuanza Mwezi Mtukufu wa Ramadhani mnamo Aprili 13. Amesema inatazamiwa kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani utakuwa na siku 30 na hivyo tarehe Mosi Shawwal inatazamiwa kusadifiana na Mei 13.