Dua hizi za kila siku za Mwezi wa Ramadhani husomwa toka mwanzo ya tarehe mosi Ramadhani hadi siku ya mwisho katika mwezi huu mtukufu. Kila dua ina siku yake, na inaweza kusomwa mara nyingi kadiri ya uwezo wa mtu mwenyewe.

Ewe Mwenyezi Mungu; Siku hii, (tafadhali) nitunuku fadhila Laylatul Qadr. Na ubadilishe mambo yangu kutoka kwa shida kuwa wepesi.
Na ukubali ombi langu la msamaha, Na niondolee dhambi zangu na mizigo yangu; Ewe Ambaye ni Mpole kwa waja Wake wema.