IQNA

Usajili Wafunguliwa kwa Tuzo ya Kimataifa ya Qur’ani ya UAE

18:59 - October 14, 2025
Habari ID: 3481367
IQNA-Idara Kuu ya Mambo ya Kiislamu, Awqaf na Zakat ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imetangaza kuanza kwa usajili wa toleo la pili la Emirates International Quran Award.

Tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya usajili ni Oktoba 31, 2025. Nyaraka zinazohitajika ni nakala ya pasipoti, fomu ya usajili iliyotiwa muhuri wa taasisi inayomtambulisha mshiriki, na picha ya kibinafsi.

Hatua ya awali ya mashindano haya itaanza Novemba 3 hadi Novemba 21, 2025. Hatua ya mwisho imepangwa kufanyika kuanzia Januari 20 hadi 30, 2026.

Masharti kwa washiriki ni kuwa wamehifadhi Qur’ani yote, kuwa na ujuzi wa Tajweed na usomaji sahihi, kuwa na sauti nzuri, na umri usiozidi miaka 35.

Washiriki lazima watambulishwe na taasisi rasmi na mashuhuri kutoka nchi wanazoishi. Maombi ya binafsi bila utambulisho rasmi hayatakubaliwa.

Washiriki lazima wawe miongoni mwa walioshinda nafasi tatu za juu katika mashindano ya kimataifa yaliyotambuliwa rasmi ndani ya kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Waombaji wote watapitia mitihani ya maandishi na ya mdomo mbele ya jopo la majaji wa kimataifa, na wanatakiwa kufuata kanuni za nidhamu na mwenendo katika hatua zote za tuzo hii.

4310483

captcha