uislamu - Ukurasa 9

IQNA

Imam Khamenei
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei, amesema kuwa, ibada ya hija ni fursa bora kabisa kwa ajili ya kukabiliana na njama za kuitenganisha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na ulimwengu wa Kiislamu na nara yake ya ‘kukabiliana na shubha na propaganda zinazoenezwa na maadui wa Uislamu’ na kutoa jibu mwafaka kwa mahitaji ya kimaanawi na kifikra za mahujaji.
Habari ID: 1465135   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/28

Spika wa Bunge la Italia amesema kuwa, dini ya Kiislamu haipaswi kufungamanishwa na vitendo vya kufurutu mipaka vinavyofanywa na makundi ya kitakfiri na kigaidi kama vile Daesh na kusisitiza kwamba jamii ya kimataifa inapaswa kuelewa kwamba misingi ya dini ya Kiislamu ni kutangaza amani na upendo na inalaani ghasia na machafuko
Habari ID: 1461624   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/19

Misikiti na vituo vya Kiislamu katika mji wa la Inland ndani ya jimbo la California, vimeendelea na juhudi zao za kuwafahamisha watu kuhusu Uislamu wa asili ambao unapenda amani na utulivu.
Habari ID: 1460941   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/17

Waziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ameyashambulia vikali makundi ya kigaidi na kitakfiri katika eneo la Mashariki ya Kati akisema kuwa makundi hayo yanaonyesha picha mbaya kwa dini tukufu ya Kiislamu.
Habari ID: 1455492   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/30

Wawakilishi wa Misri na Morocco wametia saini makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya kidini ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzefu katika sekta ya uchapishaji na usambazaji wa nakala za Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 1450407   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/15

Ayatullah Khatami
Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo mjini Tehran amesema, 'kundi la kigaidi la Daesh ni silaha mpya ya Marekani na madola mengine ya kibeberu inayotumiwa kwa lengo la kuvuruga usalama wa eneo la Mashariki ya Kati.
Habari ID: 1422882   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/06/27

Sheikhe mkuu wa Al Azhar Ahmad Tayyib amehutubu katika sherehe za ufunguzi katika sherehe za ufunguzi wa Kombe la Dunia Brazil baadaye hii leo
Habari ID: 1416916   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/06/12

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haijawahi kusalimu amri mbele ya nchi za Magharibi na kwamba imeweza kustawi na kuendelea siku hadi siku.
Habari ID: 1414443   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/06/05

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema, umoja na kuundwa umma ulio shikamana ni hitajio la dharura katika Ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 1411477   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/27

Tarehe 27 Rajab Mwaka wa Tembo na akiwa na umri wa miaka 40, Mtume Muhammad (SAW) alikuwa juu ya kilele cha Mlima Hira, akijishughulisha na ibada ndani ya pango la mlima huo, ambapo ghafla malaika Jibril AS alimteremkia huku akiwa amebeba wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu SW.
Habari ID: 1411465   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/05/27

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwaenzi na kuwaheshimu wafanyakazi na wale wote wanaohusika katika uga wa uzalishaji ni dharura ambayo imesisitizwa na Uislamu.
Habari ID: 1401876   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/04/30