Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, njama kubwa za maadui ni kuwatoa uwanjani wananchi wa Iran na kwamba Ukanda wa Gaza hivi sasa ni mfano wa wazi na wa kivitendo wa nguvu kubwa za wananchi huku akisisitiza kuwa historia haitasahau jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wanawake na watoto Wa palestina .
Habari ID: 3478174 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/09
Jitihada
IQNA - Licha ya mashambulizi ya mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Gaza ambayo yamepelekea watu ya 23,000 kupoteza maisha na malaki kuyahama makazi yao, mafunzo ya Qur'ani Tukufu yanaendelea katika eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3478163 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/07
Watetezi wa Palestina
IQNA – Makumi ya makundi na mashirika ya kijamii nchini Marekani yametangaza azma ya kushiriki katika maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika Washington, DC, kuunga mkono Wa palestina wanaodhulumiwa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478158 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/06
Jinai za Israel
IQNA - Idara ya Wakfu ya Kiislamu, inayosimamia Msikiti wa Al-Aqsa huko al-Quds (Jerusalem), imesema leo kwamba ni waumini 15,000 pekee walioruhusiwa kuingia katika eneo hilo takatifu kwa ajili ya Sala ya Ijumaa kutokana na vikwazo vilivyowekwa na utawala ghasibu wa Israel.
Habari ID: 3478154 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/05
Jinai za Israel
IQNA – Utawala katili wa Israel umefyatua zaidi ya tani 65,000 za makombora na mabomu kwenye Ukanda wa Gaza tangu Oktoba 7, 2023, na kuua takriban watu 22,438, wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
Habari ID: 3478150 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/05
Kadhia ya Palestina.
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amesema mpaka wa ulimwengu wa Kiislamu uko Gaza hivi leo, na kwamba Wa palestina wa eneo hilo wamesimama dhidi ya kiburi au mfumo wa kiistikbari na Marekani.
Habari ID: 3478140 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/03
IQNA - Idara ya Waqfu ya Kiislamu huko al-Quds (Jerusalem) imesema kumeshuhudiwa ongezeko la idadi ya walowezi wa Kizayuni waliouhujumu Msikiti wa Al-Aqsa mwaka jana.
Habari ID: 3478133 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/02
IQNA - Wanazuoni waandamizi wa Kiislamu nchini Yemen katika taarifa wamesisitiza kuwa ni Haramu kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3478131 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/02
Watetezi wa Palestina
IQNA-Afrika Kusini imefungua kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu mashambulizi ya "mauaji ya kimbari" ya utawala huo dhidi ya Gaza, ambayo hadi sasa yameua zaidi ya Wa palestina zaidi ya 21,500.
Habari ID: 3478112 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/30
Watetezi wa Palestina
IQNA - Waandamanaji kutoka matabaka mbalimbali walifanya maandamano mjini The Hague, Uholanzi kudai haki kwa Wa palestina na uchunguzi wa jinai zinazofanywa na utawala wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3478106 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/28
IQNA-Rais Miguel Diaz-Canel wa Cuba amelaani vikali mauaji ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza na kueleza kwamba, mauaji hayo ya kimbari ni kashfa na fedheha kwa ubinadamu.
Habari ID: 3478104 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/28
Watetezi wa Palestina
IQNA - Wakati wa maandamano ya wafuasi wa Palestina huko Rabat, mji mkuu wa Morocco, siku ya Jumapili, maelfu ya raia wa Morocco walitoa wito wa kukatwa uhusiano na utawala wa Kizayuni unaoendelea kutekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wa palestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478090 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/25
Watetezi wa Palestina
IQNA - Mikutano ya hadhara imefanyika katika miji katika nchi mbalimbali za Magharibi mwishoni mwa juma kupinga mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wa palestina wa Gaza na kutaka kuwasilishwa kwa misaada ya kibinadamu katika eneo lililozingirwa.
Habari ID: 3478086 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/24
Watetezi wa Palestina
IQNA-Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria chimbuko la matukio ya hivi karibuni huko Palestina na kusema kuwa, Marekani na utawala wa Kizayuni zinapaswa kushtakiwa kwa kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza.
Habari ID: 3478082 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/24
Kadhia ya Palestina
IQNA-Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema utawala wa Israel hauwezi kufanya jinai nyingi kiasi hiki dhidi ya Wa palestina huko Ghaza bila ya uungaji mkono wa Marekani na Uingereza.
Habari ID: 3478081 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/23
Kadhia ya Palestina
IQNA-Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hatimaye limepitisha azimio kuhusu jinai za Israel dhidi ya Gaza, likidai kuongezwa kwa misaada katika eneo lililozingirwa lakini lakini limeshindwa kuulazimisha utawala haramu wa Israel usitishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wa palestina katika eneo hilo.
Habari ID: 3478078 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/23
Kadhia ya Palestina
IQNA- Chama kikuu cha upinzani nchini Bahrain cha al-Wefaq kimesema hatua ya utawala wa Aal-Khalifa ya kujiunga na muungano wa baharini wa Marekani katika Bahari Nyekundu ni kusaliti kadhia ya Palestina.
Habari ID: 3478077 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/23
Chuki dhidi ya Uislamu
IQNA - Kumekuwa na ongezeko mara saba la mashambulizi ya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) nchini Uingereza kutoka Oktoba 7 hadi Desemba 13. Hayo ni kwa mujibu wa taasisi ya Tell MAMA ambayo iafuatilia matukio ya chuki dhidi ya Uislamu nchini Uingereza.
Habari ID: 3478073 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/22
Jinai za Israel
IQNA – Mji wa Al-Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala ghasibu wa Israel Ijumaa umeshuhudia vikosi vya Israel vikitumia gesi ya kutoa machozi na nguvu ziada kuwatawanya waumini karibu na eneo la Msikiti wa Al-Aqsa huku watu wengi wakiugua kwa kuvuta gesi hiyo ya machozi.
Habari ID: 3478072 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/22
Watetezi wa Palestina
IQNA - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Ansarullah nchini Yemen imetangaza kuanza mchakato wa uhamasishaji wa vijana wanaojitolea kuenda kupigana katika vita vya Gaza pamoja na wapiganaji wa harakati za Kiislamu huko Palestina.
Habari ID: 3478070 Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/21