iqna

IQNA

iran
Jinai dhidi ya Iran
TEHRAN (IQNA)- Wizara ya Intelijensia (Usalama) ya Iran imesema kuwa, vikosi vya usalama nchini vimewatia mbaroni magaidi 26 wakufurishaji ambao walihusika na shambulio la hivi karibuni la kigaidi kwenye Haram Takatifu ya Shah Cheragh katika mkoa wa kusini wa Fars na kuongeza kuwa, mratibu mkuu wa machafuko hayo hatari ni raia wa Jamhuri ya Azerbaijan.
Habari ID: 3476053    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/11/07

Ustawi wa Iran
TEHRAN (IQNA)- Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imezindua mfumo mpya wa makombora ya kujihami ya masafa marefu ya Bavar (Kujiamini) 373 na pia imefanyia majaribio kombora jipya la Sayyyad B4 leo Jumapili.
Habari ID: 3476044    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/11/06

Mwamko dhidi ya Marekani
TEHRAN(IQNA)- Washiriki katika maandamano ya Siku ya Taifa ya Kupambana na Ubeberu inayosadifiana na leo 4 Novemba, wamesisitiza udharura kuwepo mapambano endelevu dhidi ya njama za kuzusha fitna, ghasia na fujo.
Habari ID: 3476032    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/11/04

Jibu kwa jinai za Marekani
TEHRAN (IQNA)- Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa imeyaweka majina ya shakhsia kumi na taasisi nne za Marekani kwenye orodha yake ya vikwazo.
Habari ID: 3476020    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/11/01

Hujuma ya kigaidi
TEHRAN (IQNA)- Wizara ya Intelijensia (Usalama) ya Iran imetangaza kuwa, imewatambua na kuwatia nguvuni watu sita katika timu ya usaidizi ya magaidi watenda jinai dhidi ya Haram takatifu ya Ahmad bin Musa (AS) maarufu kama Shah Cheragh huko katika mji wa Shiraz.
Habari ID: 3476015    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/31

Njama dhidi ya Iran
TEHRAN (IQNA)- Wananchi wa jiji la Tehran na miji yote ya Iran, leo baada ya Sala za Ijumaa, wamefanya maandamano makubwa ya nchi nzima kulaani shambulio la kigaidi lililotokea juzi Jumatano katika Haram Tukufu ya Shah Cheragh ya mjini Shiraz, kusini magharibi mwa Iran. Genge la kigaidi la ISIS limetangaza kuhusika na jinai hiyo.
Habari ID: 3475997    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/28

Hujuma ya kigaidi
TEHRAN (IQNA)- Kufuatia tukio la kigaidi lililotokea katika Haram ya Hadhrat Ahmad bin Musa (Shah Cheragh) huko Shiraz, Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za rambirambi kwa familia zilizofiwa akisisitiza kuwa wahalifu waliohusika na jinai hiyo wataadhibiwa.
Habari ID: 3475992    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/27

Mashindano ya Qur'ani ya Iran
TEHRAN (IQNA) - Ukumbi wa Kimataifa wa Tehran utakuwa mwenyeji wa toleo lijalo la Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran.
Habari ID: 3475991    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/26

Ugaidi dhidi ya raia
TEHRAN (IQNA)- Zaidi ya watu 15 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya gaidi aliyekuwa na silaha nzito kushambulia eneo takatifu katika mkoa wa kusini magharibi mwa Iran wa Fars siku ya Jumatano.
Habari ID: 3475990    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/26

Mashindano ya Qur'ani Iran
TEHRAN (IQNA) - Mialiko imetumwa kwa zaidi ya nchi 120 kwa ajili ya kushiriki katika toleo lijalo la Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran, afisa mmoja alisema.
Habari ID: 3475981    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/24

Chuki dhidi ya Uislamu
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu wa Iran amesema, vyombo vya habari vyenye uadui vinapindua ukweli na kuandaa habari bandia ili kujaribu kutoa taswira isiyo sahihi kuhusu Iran ya Kiislamu na Ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 3475977    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/23

Iran na Ustawi
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, maendeleo ya miaka 40 ya nchi yanadhihirisha usahihi wa uchambuzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu dunia mkabala wa uchambuzi wa watu wenye fikra na mielekeo ya Kimagharibi.
Habari ID: 3475956    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/20

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu hautasalimu amri mbele ya madola yenye nguvu na kusisitiza kuwa: Jamhuri ya Kiislamu hivi sasa imekuwa mti imara uliostawi ambao ni muhali hata kufirikia kwamba unaweza kung'olewa.
Habari ID: 3475926    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/14

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametaja ghasia na machafuko yaliyoenea katika maeneo mbalimbali hapa nchini kuwa ni mpango usio wa kawaida na wa fedheha wa adui mkabala wa maendeleo na harakati za ubunifu na kubwa za taifa la Iran na kwamba njia ya kukabiliana na maadui ni kusimama imara.
Habari ID: 3475921    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/12

Wiki ya Umoja wa Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa siri ya ushindi wa nchi hii katika sekta mbalimbali ni kuwepo umoja baina ya Masuni na Mashia na kusisitiza kuwa, Waislamu wa Kisuni na pia wa Kishia waliifanya Iran kuwa imara zaidi na yenye nguvu wakati wa kujihami kutakatifu na katika matukio ya ndani kupitia umoja na dhamira yao thabiti.
Habari ID: 3475904    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/09

Umoja wa Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kongamano la 36 la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu litafanyika mjini Tehran kuanzia tarehe 17 hadi 22 Oktoba kwa kuhudhuriwa na wasomi na wanafikra kutoka sehemu mbalimbali za dunia.
Habari ID: 3475898    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/08

Khatibu wa Sala ya Ijumaa
TEHRAN (IQNA)- Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya mjini Tehran amesisitiza kuwa: Uimwengu wa Ubeberu, Ulimwengu wa Uistikbari, Marekani, Uzayuni na kambi Ukufurushaji, zinapigana vita dhidi ya na haki na uadilifu visivyosuluhishika.
Habari ID: 3475892    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/07

Mashindano ya Qur'ani
TEHRAN (IQNA)- Hafla ya kufunga Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Uturuki ilifanyika Jumatano usiku katika mji mkuu wa nchi hiyo, Ankara.
Habari ID: 3475887    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/06

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika hafla ya pamoja ya wanachuo wahitimu wa Vyuo Vikuu vya vikosi vya ulinzi nchini Iran kwamba ghasia na machafuko yaliyoshuhudiwa hivi karibuni hapa nchini yaliratibiwa na Marekani na utawala ghasibu na bandia wa Kizayuni na kusaidiwa kwa hali na mali na mabwana zao na baadhi ya wasaliti raia wa Iran wanaoishi nje ya nchi.
Habari ID: 3475872    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/03

Harakati ya Hizbullah
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi sasa ina nguvu na uthabiti kuliko wakati wowote ule, na kwamba taifa hili litavuka salama mtihani wa sasa kutokana na hekima ya viongozi wake.
Habari ID: 3475867    Tarehe ya kuchapishwa : 2022/10/02