iran - Ukurasa 9

IQNA

IQNA – Zaidi ya Wairani milioni tano wanasubiri kwa hamu nafasi yao ya kwenda kufanya ibada ya Umrah, afisa mmoja amesema.
Habari ID: 3481156   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/30

IQNA – Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani kwa Wanafunzi Waislamu yanajitahidi kuimarisha uhusiano kati ya washiriki duniani kote badala ya kuwa mashindano ya muda mfupi pekee, amebaini mtaalamu.
Habari ID: 3481148   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/28

IQNA – Hatua ya kuchagua wawakilishi wa Iran katika Mashindano ya Saba ya Kimataifa ya Qur’ani kwa Wanafunzi Waislamu imefanyika katika Shirika la Qur’ani la Wanazuoni wa Iran, Jumanne.
Habari ID: 3481141   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/26

IQNA – Mkutano wa dharura wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Kiislamu (OIC) ulianza Jumatatu mjini Jeddah, Saudi Arabia, ambapo washiriki wamesisitiza umuhimu wa hatua ya pamoja kusaidia Gaza na Palestina.
Habari ID: 3481136   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/26

IQNA – Kikundi cha kwanza cha Wairano wanaotekeleza Umrah baada ya Hajj ya mwaka huu kimewasili Madina, Saudi Arabia baada ya kuondoka mapema Jumamosi asubuhi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Imam Khomeini jijini Tehran.
Habari ID: 3481126   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/23

QNA – Msafara wa Qur’ani wa Arbaeen kutoka Iran, unaojulikana mwaka huu kama “Msafara wa Imam Ridha (AS)”, ulianza shughuli zake katika njia ya Arbaeen tarehe 8 Agosti 2025.
Habari ID: 3481109   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/20

IQNA – Awamu ya awali ya kategoria ya usomaji katika Mashindano ya 7 ya Kimataifa ya Qur'ani kwa Wanafunzi Waislamuyaliyoandaliwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeanza rasmi, huku washiriki kutoka mataifa 36 wakituma video za usomaji kwa ajili ya tathmini.
Habari ID: 3481101   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/18

IQNA – Mkurugenzi wa Msafara wa Hijja wa Iran ameifu mshikamano wa kimataifa uliodhihirika wakati wa vita vya siku kumi na mbili vilivyoanzishwa na utawala wa Israel dhidi ya Iran, na ametilia mkazo umuhimu wa umoja wa Waislamu kuelekea Siku ya Arbaeen ya Imam Hussein (AS).
Habari ID: 3481035   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/04

IQNA – Picha zilizopigwa mwishoni mwa Julai 2025 zinaonesha athari za mashambulizi ya kigaidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya mji mkuu wa Iran, Tehran, mwezi Juni, ambapo maeneo ya makaazi ya raia yalilengwa.
Habari ID: 3481033   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/08/02

IQNA – Kundi la walimu na maqarii mashuhuri wa Qur’ani kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limeandika barua ya wazi kwa maqari wa Misri, likiwataka wachukue msimamo dhabiti dhidi ya ukatili wa utawala wa Kizayuni huko Gaza na kusimama pamoja na watu wanyonge wa eneo hilo.
Habari ID: 3481022   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/30

IQNA – Afisa mmoja kutoka Wizara ya Elimu ya Iran amesema kuwa shule 1,200 za kuhifadhi Qur’ani zinapangwa kuzinduliwa nchini ili kusaidia mpango wa kuwafundisha wahifadhi milioni 10 wa Qur’ani.
Habari ID: 3481018   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/30

IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatعllah Sayyid Ali Khamenei, amesema kuwa vita vya siku 12 vilivyoanzishwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran vimeonesha kwa dhahiri uimara wa kipekee wa Jamhuri ya Kiislamu pamoja na dhamira thabiti na uwezo wake mkubwa.
Habari ID: 3481016   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/29

IQNA – Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwamba mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yameshindwa kutimiza malengo waliyojiwekea, huku akisisitiza kwamba taifa hilo litaendelea kusonga mbele kwa kasi zaidi katika nyanja za kijeshi na kielimu kwa azma iliyo imara.
Habari ID: 3481003   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/26

IQNA – Kwa mara ya kwanza baada ya karibu miongo miwili, mtaalamu wa Qur’an Tukufu kutoka Iran atahudhuria kama jaji katika mashindano ya kimataifa ya Qur’an nchini Malaysia.
Habari ID: 3480981   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/22

IQNA – Profesa Ali Montazeri, Mkuu wa Akademia ya Kitaifa cha Elimu, Utamaduni na Utafiti (ACECR) nchini Iran, amesema kuwa lengo la mashambulizi ya pamoja ya Marekani na Israel dhidi ya Iran ni kuzuia maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia ya taifa hilo.
Habari ID: 3480977   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/21

IQNA – Mkutano wa 20 wa wataalamu wa Qur’ani, makari na wahifadhi wa Iran utafanyika mwezi Novemba mwaka huu chini ya usimamizi wa Baraza Kuu la Qur’ani.
Habari ID: 3480976   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/21

IQNA – Mtaalamu kutoka chuo kikuu nchini Lebanon amesema kuwa lengo la utawala wa Kizayuni katika vita vya siku 12 dhidi ya lilikuwa kuuangusha mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusukuma mbele mpango wao wa “Mashariki ya Kati Mpya”, lakini muqawama na kusimama kidete Iran kuliuzuia.
Habari ID: 3480973   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/20

IQNA-Hatua ya Awali ya Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani kwa Wanafunzi wa Kiislamu Imeanza kwa Njia ya Mtandao
Habari ID: 3480970   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/20

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema Israel ililazimika "kusalimu amri na kuing'ang'ani Marekani" kwa kukata tamaa, wakati wa vita vya hivi karibuni vya siku 12 dhidi ya Iran, na kuthibitisha kuwa haina na uwezo wa kukabiliana na Jamhuri ya Kiislamu bila msaada.
Habari ID: 3480956   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/16

IQNA – Shirika la Kimataifa la Habari za Qur’ani limeandaa warsha ya kimtandaoni (webinar) ya kimataifa iitwayo "Hadhi na Nguvu ya Iran; Ujumbe Zaidi ya Makombora" itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii.
Habari ID: 3480952   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/07/16