“Uhusiano wa Amerika ya Latini na Uislamu ulianza karne ya 12 Miladia, Waislamu walivumbua Bara Amerika mwaka 1178, na si Christopher Columbus,” alisema Erdogan alipohutubu katika kongamano la kimatiafa la viongozi Waislamu kutoka Amerika ya Latini.
“Mabaharia Waislamu waliwasili Amerika mwaka 1178. Columbus mwenyewe alitaja kuwepo msikiti katika mlima ulio katika Pwani ya Cuba,” alisema Erdogan.
Ameongeza kuwa Uturuki iko tayari kujenga upya msikiti katika eneo hilo.
Vitabu vingi vya historia vinadai kuwa Columbus ndie aliyekuwa mtu wa kwanza wa kigeni kufika bara Amerika mwaka 1492 wakati akitafuta njia mpya ya baharini kuelekea India.../mh