IQNA

Utawala wa Kizayuni kubomoa nyumba mpya 400 za Wapalestina

9:00 - February 08, 2015
Habari ID: 2822419
Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel ameagiza kubomolewa nyumba mpya 400 za raia wa Palestina wa eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu na utawala huo.

Netanyahu amechukua hatua hiyo baada ya gazeti la Uingereza la Daily Mail kutoa ripoti iliyodai kuwa, Umoja wa Ulaya ndio uliofadhili ujenzi wa nyumba hizo za Wapalestina. Utawala wa Kizayuni wa Israel umedai kuwa Umoja wa Ulaya kwanza ulipasa kuomba kibali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo. Msemaji wa umoja wa Ulaya jana alitetea hatua ya umoja huo ya kufadhili ujenzi wa nyumba hizo mpya za raia wa Palestina. Shadi Othman afisa mawasiliano katika ofisi ya Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na Ukanda wa Ghaza juzi aliliambia gazeti la Daily Mail kuwa, mradi huo ni sehemu ya kazi iliyotekelezwa kwa minajili ya kuandaa mustakbali wa nchi ya Palestina. Othman ameongeza kuwa, Wapalestina wana haki ya kuishi huko, kujenga shule na kuwa na maendeleo ya kiuchumi.../mh

2819092

captcha