“Hilali ya Ramadhani itazaliwa Jumanne, Juni 16, 2015 saa 14:05 GMT (17:05 alasiri kwa saa za Makkah),” imesema taarifa ya baraza hilo lenye makao yake huko Dublin nchini Ireland.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, itakuwa haiwezekani kuona mwezi mwandamo wakati wa Magharibi Jumatano, Juni 17, kwa jicho au hata kwa suhula za kisasa kama vile telescope.
Kwa msingi huo, “Alkhamisi Juni 18 itakuwa siku ya kwanza ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, kwa idhini yake Allah SWT.”
Kwingineko Jumuiya ya Kiislamu ya Amerika Kaskazini (ISNA) nayo pia imetangaza kuwa, kwa mujibu wa taarifa za wataalamu , Juni 18 itakuwa tarehe mosi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika mwaka huu wa 1436 Hijria.../mh