Katika ujumbe uliotolewa siku ya Jumamosi kufuatia kuuawa
shahidi Sheikh Nimr Baqir Nimr, mwanazuoni mtajika wa Kiislamu Saudia. Huku
akilaani kitendo hicho cha utawala wa Aal Saud, Rais Rouhani ameongeza hakuna
shaka kuwa kitendo hicho cha serikali ya Saudi Arabia kitapelekea utawala huo
kuchukiwa zaidi duniani hasa katika nchi za Kiislamu.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kitendo hicho cha Saudia Arabia cha
kumuua Sheikh Nimr pia kitachangia katika kuvuruga uthabiti wa eneo, kuibua
vita na machafuko.
Rais Rouhani katika ujumbe huo amesema, hata kama Waislamu nchni Iran
wanajiunga na Waislamu kote duniani katika kulaani kitendo hicho kilicho dhidi
ya ubinadamu, lakini hawataruhusi jinai hii itumiwe na baadhi ya watu kuchukua
hatua za kuvunja sheria na kuvunja hadhi ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran.
Ikumbukwe kuwa siku yua Jumamosi, Wizara ya Mambo ya Ndani Saudi Arabia
ilitangaza kuwa Sheikh Nimr Baqir Al Nimr mwanazuoni maarufu wa Kiislamu na
mtetezi wa haki za binadmau ameuawa kufuatia amri ya mahakama. Jinai hiyo
imelaaniwa vikali na viongozi, shakhsia wa kisiasa na kidni kote duniani.
3464155