Maandamano yamefanyika nje ya Ubalozi wa Saudi Arabia mjini Berlin, Ujerumani ambapo washiriki wameilaani Saudia kwa kuendelea kutoa misaada kwa kundi la kigaidi la Daesh au ISIS.
Waandamanaji hao waliokuwa na hasira wamelaani uungaji mkono wa Saudia kwa magaidi huko Syria, Iraq, Yemen na nchi zingine duniani.