IQNA

Makundi ya Palestina

Matokeo ya uchaguzi wa bunge Israel yanayonyesha kura kwa ubaguzi

16:36 - March 03, 2020
Habari ID: 3472526
TEHRAN (IQNA) –Makundi ya muqawama au kupigania ukombozi wa Palestina yamesisitiza kuwa, matokeo ya awali ya uchaguzi wa bunge katika utawala wa Kizayuni wa Israel yanayoneysha kuwa hakuna mabadiliko yoyote katika sera za utawala huo.

Makundi hayo ya kupigania ukombozi Palestina yamesisitiza kuwa, matokeo hayo ya uchaguzi  yanayonyesha kuwa utawala wa Kizayuni unakusudia kuendeleza sera zake za ubaguzi na apatheidi dhidi ya watu wa Palestina.

Katika taarifa, Fauzi Barhoum, Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina amesema,  mapambano ya kupigania ukombozi wa Palestina yataendelea bila kujali ni serikali gani inayochukua madaraka Israel.

Naye Dawud Shahab mmoja kati ya makamanda wa Harakati ya Jihad Islami amesema matokeo ya uchaguzi wa bunge la Israel hayabadilisho ukweli wowote kwani ardhi za Palestina zinaendelea kukaliwa kwa mabavu na hivyo mapambano yanapaswa kuendelea dhidi ya Wazayuni maghasibu. Naye Mustafa Al Bargouthi, Katibu Mkuu wa  Harakati ya Ubunifu wa Kitaifa Palestina anasema matokeo ya uchaguzi wa bunge la Israel yanaonyesha kupata uungaji mkono wanasisia wabaguzi na wenye misimamo mikali. Ameongeza kuwa nukta hiyo inaonyesha kuwa jamii ya Israel inaunga mkono ubaguzi na mfumo wa apatheidi katika utawala huo bandia.

3882872

captcha