IQNA

Sala ya Tarawih ni marufuku Oman katika Mwezi wa Ramadhani

21:58 - April 05, 2021
Habari ID: 3473785
TEHRAN (IQNA)- Sala ya Tarawih imepigwa marufuku nchini Oman kwa lengo la kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona huku sheria ya kutotoka nje usiku ikitekelezwa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Kwa mujibu wa tovuti ya royanews.tv Kamati Kuu ya Kupambana na COVID-19 nchini Oman Jumatatu imetangaza kuwa,  Sala ya Tarawih ni marukufu katika misikiti yote nchini humo.

Halikadhalika kamati hiyo imetangaza sheria ya kutotoka nje kuanzia kuanzia saa tatu usiku hadi saa 10 alfajiri kuanzia Aprili 8.

Kamati Kuu ya Kupambana na COVID-19 nchini Oman pia imetangaza marufuku ya mijumuiko yote  ya futari au shughuli zingine misikitini na maeneo mengine katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

3962691

captcha