Ziyad al-Nakhalah aliashiria kushindwa kwa baadhi ya tawala za Kiarabu kudhoofisha harakati za mapambano ya Kiislamu kwa kurejesha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni, Al-Ahed News iliripoti.
Amesema wametambua kuwa watu wa Palestina ambao wamezingirwa wanaweza kupinga uvamizi huo na kupambana na adui.
Ameongeza kuwa, miongoni mwa nchi za Kiislamu, Iran pekee ndiyo inayolipa gharama ya kuiunga mkono Palestina.
Katika ulimwengu huu ambao umejaa dhuluma, Iran imesimama upande wa watu wa Palestina na inaendelea kuwaunga mkono, alisema.
Kwingineko katika matamshi yake, Nakhalah amesisitiza ulazima wa kuwepo umoja zaidi kati ya makundi ya Wapalestina na kuimarishwa muqawama dhidi ya utawala wa Kizayuni.