IQNA

Hamasi : Operesheni ya Kimbunga Cha ya Al-Aqsa ni Pigo la Kimkakati kwa Maadui

11:22 - October 17, 2023
Habari ID: 3477748
AL-QUDS (IQNA) - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamasi Ismail Haniyeh alielezea Operesheni ya Kimbunga cha ya Al-Aqsa iliyoanzishwa na vikosi vya upinzani huko Gaza dhidi ya utawala wa Kizayuni kama kushindwa kwa kimkakati kwa Maadui.

Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamasi Ismail Haniyeh alisema utawala wa Israeli hauna uwezo wa kukabiliana na muqawama wa Palestina na ndio maana umeanza kutekeleza mauaji ya raia, iliripotiwa na Al-Mayadeen.  

Wazayuni walianzisha kampeni ya mauaji na uhamisho wa raia ili kufidia kushindwa kwao na pigo walilopata kutokana na operesheni kimbunga cha Al-Aqsa mwezi Oktoba 7, alisema.  

Haniye alivipongeza vikosi vya upinzani kwa kuanzisha operesheni hiyo ambayo inachukuliwa kuwa mwanzo wa kupungua kwa uvamizi huo.  

Pigo la kimkakati lililotolewa kwa wavamizi ni dhibitisho kwamba ukombozi wa ardhi yetu unaweza kufikiwa, na  alibainisha.  

Tutaendeleza mkakati wa ukombozi na kurudi licha ya hatua za adui na uungwaji mkono wa pande zote kwa Israeli kutoka Marekani na  Nchi za Magharibi.

Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Ushindi Kabisa kwa Upinzani Islamic Jihadi

Haniyeh alitupilia mbali zaidi wazo la kuwatuma watu wa Gaza nchini Misri, akisema hakutakuwa na uhamiaji kutoka Ukanda wa Gaza.  

Uamuzi wa kuwaondoa watu wa Gaza kutoka katika ardhi yao utaisha bila mafanikio, alisema.  

Afisa huyo wa Hamas pia amewashukuru wale wote ambao wameunga mkono muqawama wa Palestina dhidi ya kukaliwa kwa mabavu na kutoa wito wa kuendelezwa uungaji mkono huo.  

Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan pia unapaswa kubaki amilifu kwa sababu sisi sote ni taifa moja na sote tunataka wavamizi waondoke katika ardhi yetu na tunataka kuanzisha nchi huko Palestina na mji mkuu wa al-Quds.

Hamas ilianzisha mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba, Shambulizi hilo lililopewa jina la Operesheni yakimbunga cha  Al-Aqsa, lilihusisha shambulio la ardhini na angani kwenye makazi ya Waisraeli karibu na Ukanda wa Gaza, pamoja na shambulio kubwa la roketi katika miji ya Tel Aviv. Ashkeloni, na wengine Wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa shambulizi hilo lilitoa pigo kubwa kwa utawala wa Israel na serikali ya Benjamin Netanyahu.

Operesheni hiyo ilishtua vyombo vya usalama na kijeshi vya serikali, ambavyo vilishindwa kutarajia au kuzuia.  

Wapiganaji wa muqawama wa Palestina wametangaza kuwa operesheni hiyo ni jibu kwa dhulma, ukaliaji kwa mabavu na kuvunjiwa heshima Msikiti wa al-Aqsa unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel na walowezi wake kwa miaka mingi.  

Kwa kushtushwa na operesheni ya Palestina, utawala ghasibu wa Israel umeanzisha kampeni ya mauaji na uharibifu katika Ukanda wa Gaza na kuua mamia ya watu wasio na hatia na kuharibu nyumba, shule, hospitali na miundombinu ya eneo hilo.

 

3485579

 

 

 

captcha