IQNA

Chuki dhidi ya Uislamu

Kikao cha kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu

9:07 - March 10, 2024
Habari ID: 3478479
IQNA - Baku, mji mkuu wa Jamhuri ya Azerbaijan, inaandaa mkutano wa kimataifa wa kitaalmu unaoitwa "Kukumbatia Anua ya Jamii: Kukabiliana na Chuki dhidi ya Uislamu mwaka 2024".

Mkutano huo umefanyika kwa mnasaba wa mwaka wa pili wa  maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kukabiliana na Chuki Dhidi Uislamu (Islamophobia).

Mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja na Kituo cha Kimataifa cha Utamaduni cha Kimataifa cha Baku (BIMC), Kituo cha Uchambuzi wa Mahusiano ya Kimataifa (Kituo cha AIR), Jukwaa la Dini la G20, na Kundi la Ubunifu wa Baku.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Kiislamu ya Pakistan Sultan Ahmad Ali ni mmoja wa washiriki wa mkutano huo

Katika hotuba yake, alisema kuwa katika kipindi cha miaka 20 iliyopita, kumekuwa na ongezeko kubwa la chuki dhidi ya Uislamu katika nchi za Magharibi.

Hii inalazimu juhudi za pamoja ili kupambana na jambo hili, alisema.

Sultan Ahmad Ali ameongeza kuwa mataifa ya Magharibi kwa kiasi kikubwa yameukanusha Uislamu.

"Tunapaswa kuunganisha juhudi zetu za kupambana na chuki dhidi ya Uislamu," alisema.

3487489

captcha