IQNA

Harakati za Qur'ani

Balozi wa Iran atembelea Kituo cha Uchapishaji Qu’ani cha Mfalme Fahd Mjini Madina

21:27 - October 23, 2024
Habari ID: 3479635
IQNA - Alireza Enayati, Balozi wa Iran nchini Saudi Arabia, ametembelea Kituo cha Uchapishaji Qu’ani cha Mfalme Fahd mjini Madina.

Katika ziara hiyo ya Jumatatu, balozi wa Iran na ujumbe wake walifahamishwa kwa kina shughuli za kituo hicho, ambapo walitazama hatua mbalimbali za uchapishaji wa Qur'ani na teknolojia inayotumika katika mchakato huo.
Enayati alipongeza juhudi na kujitolea kiwanda hicho  katika kuchapisha nakala za Qur’ani Tukufu.
Kituo cha Uchapishaji Qu’ani cha Mfalme Fahd, lililoko Madina, linasifika kwa utayarishaji wake wa kina wa Qur’ani Tukufu.
Kituo cha Uchapishaji Qu’ani cha Mfalme Fahd kilianzishwa mwaka wa 1984, na huchapisha takriban nakala milioni 10 za Qur’ani kila mwaka, na nakala hizo hujumuisha tafsiri katika lugha nyingi kama vile Kiingereza, Kiindonesia, Kirusi, Kijapani, Kiajemi, Kiurdu, Kiswahili, Kibengali na Kikorea.

3490391

captcha