Mamlaka ya Utunzaji wa Misikiti Miwili Mitakatifu ilisema kwamba kila sehemu ya kutoka imepewa rangi ya kipekee ili kuwasaidia wageni kupata njia ya kuzunguka msikiti huo mkubwa na kurudi kwenye makazi yao baada ya kumaliza Swala na ibada, vyombo vya habari vya Saudi viliripoti Jumamosi.
Mbali na kuboresha ufikiaji, kituo cha kuwatunza watoto kimeanzishwa katika ua wa msikiti ili kuwasaidia wazazi wakati wa ziara yao. Kituo hiki hufanya kazi kila siku kutoka 11 asubuhi hadi tano usiku, chini ya uangalizi wa kitaalamu.
Waziri wa Hajj na Umra wa Saudia Tawfik Rabiah alielezea madhumuni yake katika chapisho kwenye X: "Kituo cha Ukarimu kwa Watoto katika ua wa Msikiti wa Mtume hutoa nafasi salama na ya burudani yenye maudhui ya kitamaduni, kuruhusu wazazi kuppata wakati wa kutosha wa utulivu wa ibada."
Msikiti wa Mtume, iliko Al Rawda Al Sherifa, ambapo kaburi la Mtume Muhammad (SAW) lilipo, uliwakaribisha waumini zaidi ya milioni 280 mwaka 2023. Mahujaji wengi hutembelea msikiti huo baada ya kufanya Umra huko Makka, na kuifanya kuwa sehemu muhimu ya kiroho ya safari.
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa zaidi ya Waislamu milioni 10 wameswali katika Al Rawda Al Sherifa mwaka huu, ikiwa ni ongezeko la 26% kutoka mwaka uliopita, kulingana na mamlaka ya Saudia.
3490802