Uongozi wa Masuala ya Kidini wa Msikiti Mtakatifu wa Makka na Al Masjid An Nabawi au Msikiti wa Mtume (SAW), kupitia Idara ya Miduara ya Qur’ani Tukufu na Mutoon, umetangaza uzinduzi wa warsha hii kama sehemu ya programu zake za kielimu kwa lengo la kueneza elimu ya Qur’ani na kukuza utaalamu maalumu katika fani ya Qira’at.
Warsha hiyo ilianza rasmi tarehe 21 Julai 2025, na itafanyika kila siku ya Jumatatu baada ya Swala ya ‘Isha katika Msikiti wa Mtume (SAW). Washiriki watakaohudhuria kwa ukamilifu watapewa cheti rasmi cha ushiriki kilichothibitishwa na uongozi husika.
Uongozi huo umealika wale wote wenye hamu na mapenzi ya kujifunza Qira’at na elimu ya Qur’ani kufuatilia akaunti rasmi za mitandao ya kijamii ili kupata taarifa za usajili.
3493950