IQNA

Saudi Arabia yazindua usajili wa wa Itikafu Katika Misikiti Miwili Mitakatifu

21:48 - March 02, 2025
Habari ID: 3480289
IQNA – Mamlaka ya Jumla ya Saudia ya Huduma za Mambo ya Msikiti Mkuu wa Makka, Masjidul al Haram na Msikiti wa Mtume, Al Masjid an Nabawi, imetangaza kwamba usajili wa itikafu kwenye maeneo hayo mawili matakatifu utaanza Jumatano, Machi 5.

Waumini wanaotaka kushiriki katika  wakfu katika siku kumi za mwisho za Ramadhani wanaweza kuomba mtandaoni kupitia tovuti rasmi ya mamlaka hiyo, kama ilivyoripotiwa na Saudi Gazette Jumapili.

Mamlaka ilisema kuwa usajili utafungwa mara tu nafasi zote zilizotengwa zitakapojazwa.

Itikaf katika Msikiti Mkuu wa Makka na Msikiti wa Mtume huko Madina itaanza tarehe 20 ya Ramadhani (Machi 20) na itaendelea hadi mwisho wa mwezi mtukufu.

Waombaji waliokubaliwa watapata vibali rasmi kupitia tovuti, kulingana na vigezo maalum na masharti yaliyo wekwa na mamlaka.

Itikaf ni ibada ya Kiislamu ambapo waumini wanajitolea kwa sala, kusoma Qur’ani, na kutafakari kiroho ndani ya msikiti.

Kwa kawaida huadhimishwa katika siku kumi za mwisho za Ramadhani, ibada hii inafuata mfano wa Mtume Muhammad (SAW) na inachukuliwa kuwa njia ya kuimarisha uhusiano na Mungu.

Ramadhani, mwezi mtukufu zaidi katika Uislamu, ulianza Saudia mnamo Machi 1 mwaka huu.

3492105

Habari zinazohusiana
captcha