IQNA

Sehemu ya chini ya Kiswah ya Kaaba yainuliwa, Waumini waaendelea kuwasili kwa ajili ya Hija

16:55 - May 14, 2025
Habari ID: 3480687
IQNA – Katika maandalizi ya ibada ya Hija ijayo, maafisa wa Msikiti Mtakatifu wa Makka wameinua sehemu ya chini ya pazia la Kaaba, linalojulikana kama Kiswah, kwa urefu wa mita tatu.

Kwa mujibu wa Urais Mkuu wa Masuala ya Msikiti Mtakatifu wa Makka na Msikiti wa Mtume (SAW), hatua hii ni sehemu ya taratibu za kawaida za kuwapokea mahujaji kwa msimu wa Hija wa mwaka 1446 Hijria.

Mchakato huo unahusisha kukunja na kufunga sehemu ya chini ya Kiswah, kuiinua hadi mita tatu kutoka ardhini, kisha kufunika sehemu iliyo wazi kwa kitambaa cheupe cha pamba chenye upana wa takriban mita mbili.

Desturi hii ya kila mwaka hufanywa ili kulinda Kiswah dhidi ya kuguswa au kuharibika wakati wa Hija, hasa kutokana na idadi kubwa ya waumini wanaofanya Tawaf (ibada ya kuizunguka Kaaba).

Kuinyanyua Kiswah kunasaidia kuhifadhi uimara na heshima ya kitambaa hicho katikati ya misongamano ya Mahujaji.

Timu maalumu za kitaalamu huendesha shughuli hii kwa kufuata viwango vya usalama na kwa heshima ya hali ya juu kwa utakatifu wa eneo hilo.

Kaaba, iliyoko katikati ya Msikiti Mtakatifu wa Makka, ndiyo mahali patakatifu zaidi katika Uislamu na kitovu cha ibada ya Hija, ambayo huvutia mamilioni ya Waislamu kutoka kila kona ya dunia kila mwaka.

3493088

Kishikizo: pazia kaaba
captcha