Mushahara ametumikia kifungo cha miaka 23 katika magereza ya utawala ghasibu wa Israel."Nilikuwa gerezani kwa miaka ishirini na tatu, maisha yalimejaa maelezo na visa vingi, lakini namshukuru Mungu kwani muda ulipita haraka. Sikupata nafasi ya kufikiria maisha nje ya gereza. Siku zangu zilijaa masomo, ufundishaji na kujifunza. Kama wavamizi wasingenichukua mateka, nisingeweza kutoka gerezani nikiwa na kitabu hiki."
Wazo la kitabu hiki lilitokana na hitaji halisi ambalo Mashahara alilipitia ndani ya familia yake. Alipoanza kuhifadhi Qur'ani pamoja na wenzake, walikumbana na changamoto kubwa kuhusu aya zinazofanana sana (Mutashabih). Hali hii ilimfanya afanye utafiti wa kina na kupitia vitabu mbalimbali hadi akapata wazo la Qur'ani maalum kwa wanaokariri. Aliendelea kuboresha wazo hili kwa miaka kumi.
Mushahara pia ameoa heshima kwa kiongozi wa zamani wa Hamas, Yahya Sinwar, aliyeuawa shahidi mwaka uliopita. Alipokuwa gerezani, Mushahara alijifunza sarufi na muundo wa Qur'ani kutoka kwa shahidi Sinwar, jambo lililomsaidia kuelewa maana ya Qur'ani kwa mtazamo tofauti.
Mushahara ana matumaini kuwa kitabu chake kitawasaidia wote wanaotaka kuhifadhi Qur'ani.
3492925