shahidi - Ukurasa 3

IQNA

IQNA- Katika barua ya wazi iliyotumwa kwa wasomaji wa wahafidhi na wanaharakati wa Qur’ani Tukufu kutoka kote ulimwenguni, maqari na wataalamu wa Qur’ani kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameashiria mashambulizi yanayoendelea ya Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran na kusema: “Leo, Qur’ani Tukufu inatuita kwenye wajibu na hatua.”
Habari ID: 3482070    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/18

IQNA-Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuuawa shahidi kwa katibu wake, Ali Larijani, kufuatia shambulio la maadui, ambao ni Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3482069    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/18

IQNA – Msemaji wa harakati ya muqawama ya Iraq, al‑Nujaba, ameeleza mapambano yanayoendelea katika eneo la Asia Magharii kuwa ni mvutano kati ya nguvu za ukafiri na mhimili wa heshima na utukufu.
Habari ID: 3482066    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/17

IQNA – Watoto wa Iran hawaogopi wavamizi, bali wanamdhihaki adui.
Habari ID: 3482065    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/17

IQNA-Katika taarifa yenye vipengele sita iliyoelekezwa kwa serikali za nchi za Kiislamu, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema: “Lazima muamue msimamo wenu katika Vita vya Ramadhani, je, mnasimama upande wa nchi ya Kiislamu ya Iran, au upande wa Marekani na Israel?”
Habari ID: 3482064    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/17

IQNA-Gazeti moja la Marekani limekiri uwezo wa kijeshi wa Iran wa kuathiri uchumi wa dunia kwa kudhibiti Mlango-Bahari wa Hormuz.
Habari ID: 3482061    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/16

IQNA – Wakati mashambulizi ya kijeshi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yakiingia katika juma lake la tatu na idadi ya raia wanaopoteza maisha ikiongezeka pande zote mbili, sauti ya kwanza ya kupinga imejitokeza kutoka ndani ya utawala wa Trump wenyewe.
Habari ID: 3482059    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/15

IQNA-Makao Makuu ya Kamandi ya Kati ya Marekani (CENTCOM) yametangaza ‘kuanguka’ kwa ndege yao ya kijeshi ya kujaza mafuta angani katika eneo la magharibi mwa Iraq, na kutaja tukio hilo kuwa eti ni “ajali”. Hatahivyo Harakati ya Muqawama au Mapambano ya Kiislamu nchini Iraq imetangaza rasmi kutungua ndege hiyo ya jeshi la kigaidi la Marekani.
Habari ID: 3482054    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/13

IQNA-Sheikh Ahmed bin Hamad Al Khalili, Mufti Mkuu wa Oman, ametoa pongezi zake kufuatia kuchaguliwa kwa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kuwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482053    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/13

IQNA-Ayatullah Sayyid Husseini Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametoa ujumbe wake wa kwanza tangu alipochaguliwa kushika wadhifa huo muhimu.
Habari ID: 3482051    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/12

IQNA – Katibu Mkuu wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem, katika ujumbe wake amempongeza Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei na kuapa utiifu kwake.
Habari ID: 3482049    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/12

IQNA – Ofisi ya mwanazuoni mkuu wa Kishia nchini Iraq, Ayatullahil Udhma Sayyid Ali al‑Sistani, imetuma ujumbe wa kumtakia mafanikio Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu Iran, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei.
Habari ID: 3482048    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/12

IQNA-Hafla ya mazishi ya Ma shahidi wa Vita vya Ramadhani imefanyika kuanzia Uwanja wa Mapinduzi (Maidan-e Enqelab) hadi Mi‘raj al-Shuhadaa jijini Tehran, ikiambatana na mahudhurio makubwa ya wananchi waliokuja kutoa heshima zao za mwisho. Hafla hiyo imefanyika sambamba na kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Ali (AS) katika siku ya 21 ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3482047    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/12

IQNA-Mwanazuoni mashuhuri wa Ahlus-Sunna nchini Pakistan ametaja kwa sifa kubwa ubora wa kijeshi na kiuwezo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, licha ya kupita siku 11 tangu kuanza kwa uvamizi wa kijeshi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Amesema: Wavamizi bado wako katika ndoto ya ushindi, lakini Iran imevunja kiburi cha bandia cha ngome za Marekani na Israel.
Habari ID: 3482045    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/11

IQNA-Mufti Mkuu wa Russia ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kidini ya Waislamu wa Shirikisho la Russia ametuma ujumbe akimpongeza Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi Mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3482044    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/11

Uchambuzi wa Mapambano Dhidi ya Uzayuni katika Qur’ani/5
IQNA – Kwa mujibu wa aya za Surah Al-Fath na Al-Ahzab katika Qur’ani Tukufu, Mwenyezi Mungu Mtukufu amekusudia kwamba kila wakati maadui wanapoanzisha uhasama, na upande wa haki ukadumu thabiti, basi kurudi nyuma na kushindwa kwa mhalifu huwa ni jambo lisilokwepeka na lisilobadilika.
Habari ID: 3482043    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/11

Uchambuzi wa Mapambano Dhidi ya Uzayuni katika Qur’ani/6
IQNA – Qur’ani Tukufu inabainisha kwamba kiwango cha imani ya mtu kwa Mwenyezi Mungu ndicho kinachoamua kiwango cha uwezo wake wa kutenda.
Habari ID: 3482040    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/10

IQNA – Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Iraq amepongeza kuchaguliwa kwa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kuwa Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3482039    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/10

IQNA – Maandamano makubwa ya wananchi yalifanyika kote nchini Iran, yakiwemo katika mji mkuu Tehran, Jumatatu tarehe 9 Machi 2026, ambapo wananchi walitangaza utii na uungaji mkono wao kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei. Hizi hapa baadhi ya picha za maandamano hayo.
Habari ID: 3482038    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/10

IQNA – Sultani wa Oman amemtumia pongezi Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Habari ID: 3482037    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/10