shahidi - Ukurasa 4

IQNA

IQNA-Rais wa Russia, Vladimir Putin, amefanya mazungumzo ya simu na Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian kuhusu matukio ya hivi karibuni katika eneo, ambapo Rais wa Iran amesisitiza kuwa: “ Njia yetu ni kujihami kwa nguvu ili kulinda mipaka yetu na kuleta amani endelevu.
Habari ID: 3482022    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/07

IQNA – Katika siku za karibuni, Wairani katika miji mbalimbali, ikiwemo Ahvaz kusini-magharibi mwa nchi, wamefanya mikutano ya hadhara kulaani uchokozi wa Marekani na Israel, na kuelezea uungaji mkono wao kwa operesheni ya kijeshi ya kulipiza kisasi ya Iran, inayojulikana kama Operesheni ya Ahadi ya Kweli 4.
Habari ID: 3482021    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/06

Uchambuzi wa Mapambano Dhidi ya Uzayuni katika Qur’ani/1
IQNA-Qur’ani Tukufu, pamoja na kuonyesha takwimu na uchambuzi wa mambo kwa mtazamo wa kidunia, pia inatuwekea mbele mtazamo mwingine wa kutafakari kuhusu mapambano.
Habari ID: 3482020    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/06

IQNA —Chama cha Wanazuoni wa Yemen kimesema kuwa kuisaidia Jamhuri ya Kiislamu ya Iran pamoja na Harakati ya Hizbullah ya Lebanon ni wajibu wa kidini (wajib).
Habari ID: 3482019    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/06

IQNA — Wakati mashambulizi ya pamoja ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yakiendelea, Mufti Mkuu wa Libya ametangaza kuunga mkono Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482017    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/06

IQNA-Naibu Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amesema kuwa hujuma ya kijeshi yaliyotumika na Marekani na Israel dhidi ya Iran inakiuka Kanuni za Umoja wa Mataifa.
Habari ID: 3482015    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/05

IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika ujumbe wake kwa viongozi wa nchi rafiki na majirani kwamba mashambulizi ya kijeshi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel yameiacha Iran bila chaguo lolote isipokuwa kujilinda.
Habari ID: 3482014    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/05

IQNA – Kiongozi Mkuu wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Iraq, Ayatullah Sayyid Ali al-Sistani, amekemea kwa nguvu hujuma ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Iran, ambayo ilianza Jumamosi na hadi sasa imesababisha mamia kufa shahidi , wakiwemo watoto.
Habari ID: 3482013    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/04

IQNA– Sheikh Ibrahim Zakzaky, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria ametuma salamu za rambi rambi kufuatia kuuawa shahidi Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
Habari ID: 3482012    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/04

IQNA – Watu walifanya maandamano katika maeneo mbalimbali ya Bahrain, wakionyesha mshikamano wao na Iran na kutaka kulipiza kisasi kwa mauaji ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Ayatullah Seyed Ali Khamenei (Mwenyezi Mungu Amrehemu).
Habari ID: 3482011    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/03

IQNA – Mwanazuoni mmoja wa Misri amempongeza Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi , Ayatullah Seyed Ali Khamenei, na kusisitiza kwamba njia yake lazima iendelezwe na Umma ya Waislamu.
Habari ID: 3482010    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/03

Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Raji’un.
IQNA-Kufuatia shambulio la kikatili la utawala wa Kizayuni na Marekani, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ameuawa shahidi .
Habari ID: 3482006    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/01

IQNA –Mazishi ya Shahidi Haytham Ali Tabatabai, kamanda mwandamizi wa Hizbullah, pamoja na wapiganaji wengine wa muqawama waliouawa, yamefanyika Jumatatu katika kitongoji cha Beirut.
Habari ID: 3481567    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/25

IQNA – Hafla maalum ya kuadhimisha kumbukumbu ya kuuawa shahidi kwa viongozi wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imepangwa kufanyika wiki hii katika haram tukufu ya Hazrat Masoumeh (SA) huko Qom.
Habari ID: 3481307    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/30

IQNA – Harakati ya Muqawama au Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah imetangaza ratiba ya shughuli za kuadhimisha kumbukumbu ya kuuawa shahidi kwa viongozi wake mashuhuri, Sayyid Hassan Nasrallah na Sayyid Hashem Safieddine.
Habari ID: 3481249    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/17

IQNA – Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amemsifu Shahidi Rais Ebrahim Raisi kama mtumishi wa umma aliyejitolea, ambaye unyenyekevu wake na kujituma bila kuchoka kwa ajili ya watu vilimtofautisha na wengine.  
Habari ID: 3480714    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/20

IQNA – Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) ya Palestina Hamas ililaani mauaji ya Salah al-Badrawil yaliyofanywa na utawala katili wa Israel, ikisisitiza kuwa kwa kila shahidi , mwenge wa Muqawama unazidi kuwa mkali.
Habari ID: 3480421    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/23

IQNA – Mazishi ya Shahidi Sayed Hassan Nasrallah si tukio la kupita tu, bali ni u shahidi kwamba mashujaa hawafi bali wanakuwa wahusika wa kudumu na kuishi katika kumbukumbu za watu.
Habari ID: 3480257    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/23

Muqawama
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu na ujumbe maalumu kwa mnasaba wa kufanyika mazishi na maziko ya Mwanajihadi mkubwa Shahidi Sayyid Hassan Nasrullah na Shahidi Sayyid Hashem Safiyyuddin na kusisitiza kuwa: "adui ajue kwamba, Muqawama wa kukabiliana na ughasibu, dhulma na uistikbari si wa kumalizika; na kwa idhini ya Allah utaendelea hadi ufikie lengo ulilokusudia".
Habari ID: 3480256    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/23

IQNA – Wageni rasmi na wasio rasmi kutoka nchi mbalimbali wamewasili katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut, kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa katibu mkuu wa Hizbullah, Sayed Hassan Nasrallah.
Habari ID: 3480255    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/22