saudi arabia - Ukurasa 9

IQNA

TEHRAN (IQNA) -Kundi la kwanza la Waislamu wanaotekeleza Ibada ya Umrah limeingia leo katika Msikiti Mtakatifu wa Makka nchini Saudi Arabia kwa ajili ya Ibada ya Umrah baada ya ibada hiyo kufungwa kwa zaidi ya miezi sita kutokana na janga la corona.
Habari ID: 3473230    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/04

TEHRAN (IQNA) - Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nchi za Nje ya Iran amejibu madai ya uongo yaliyotolewa na Saudi Arabia ikisema kuwa imenasa kundi la magaidi lenye mfungamano na Iran na kusema: Watawala wa Saudia wanapaswa kuchagua njia ya ukweli hekima na busara badala ya kueneza uzusha na imlaa wanazopewa na madola mengine.
Habari ID: 3473217    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/30

TEHRAN (IQNA)- Jeshi la Yemen likishirikiana na vikosi vya kujitolea vya wananchi limetekeleza shambulizi la ulipizaji kisasi dhidi ya kambi ya kijeshi ya Saudi Arabia na kuangamiza askari wasipopungua 10 wa kambi ya adui.
Habari ID: 3473201    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/24

TEHRAN (IQNA) - Mkutano wa 13 wa Baraza la Kimataifa la Mwamko wa Kiislamu umefanyika katika mji mkuu wa Iran, Tehran kwa lengo la kujadil namna nchi kadhaa za Kiarabu zilivyowasaliti Wapalestina kwa kuanzisha uhusiano na utawala dhalimu wa Israel unaokalia ardhi za Palestina kwa mabavu.
Habari ID: 3473177    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/17

Kiongozi wa Ansarullah nchini Yemen
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amewakosoa vikali watawala wa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kusema tawala hizo mbili ni wabebe bendera ya unafiki, upotoshaji katika umma wa Kiislamu na wavurugaji umoja wa umma wa Kiislamu
Habari ID: 3473171    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/15

TEHRAN(IQNA)- Saudi Arabia inatafakari kuanzisha tena Ibada ya Umrah baada yakuisitisha kwa miezi kadhaa sasa.
Habari ID: 3473167    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/14

Waziri Mkuu wa Yemen
TEHRAN (IQNA) - Waziri Mkuu wa Serikali ya Uwokozi wa Kitaifa ya Yemen amekosoa hatua ya Umoja wa Mataifa ya kuiondoa Saudi Arabia katika orodha ya wauaji wa watoto.
Habari ID: 3473060    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/08/12

TEHRAN (IQNA) – Kupunguzwa kwa kiasi kikubwa idadi ya Waislamu waliotekeleza ibada ya Hija mwaka huu kumeathiria vibaya sana uchumi wa Somalia ambapo hutegemea uuzaji wa mamilioni ya mifugo nchini Saudia wakati wa Hija.
Habari ID: 3473022    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/08/01

TEHRAN (IQNA) – Waislamu wamewasili katika mji mkuu wa Makka, kwa ajili ya kutekeleza ibada ya Hija.
Habari ID: 3473003    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/26

TEHRAN (IQNA) – Mfalme Salman wa Saudi Arabia amelazwa hospitalini katika mji mkuu wa nchi hiyo, Riyadh kutokana na matatizo ya kibofu cha nyongo.
Habari ID: 3472981    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/20

TEHRAN (IQNA) – Wakuu wa ufalme wa Saudi Arabia wametangaza protokali na kanuni za kiafya zitakazotumika katika ibada ya Hija mwaka huu ili kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona.
Habari ID: 3472934    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/06

TEHRAN (IQNA) - Mahakama moja nchini Uturuki leo imeanza kusikiliza kesi ya maafisa 20 wa utawala wa Saudi Arabia waliohusika na mauaji ya mwandishi wa habari raia wa nchi hiyo Jamal Khashoggi.
Habari ID: 3472924    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/07/03

TEHRAN (IQNA) – Msomi na mhadhiri wa chuo kikuu nchini Kuwait ameibua utata katika mitandao ya kijamii baada ya kusema hatua ya Saudia wa kupunguza idadi ya mahujaji mwaka huu itaubadilisha Msikiti Mtakatifu wa Makka, Al Masjid al Haram, kuwa sawa na jumba la makumbusho.
Habari ID: 3472898    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/25

TEHRAN (IQNA) - Ufalme wa Saudi Arabia umetangaza rasmi kwamba ibada ya Hija mwaka huu itatekelezwa na watu wachache sana ambao ni raia na wakazi wa nchi hiyo.
Habari ID: 3472890    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/23

TEHRAN (IQNA) – Msikiti mmoja nchini Saudi Arabia katika eneo la Dammam umebuni nakala ya Qur'ani ya kidijitali kwa wanaoingia katika msikiti huo.
Habari ID: 3472888    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/22

TEHRAN (IQNA) - Saudi Arabia inatafakari kufuta ibada ya Hija mwaka huu kutokana na kuenea janga la corona au COVID-19.
Habari ID: 3472862    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/13

TEHRAN (IQNA)- Naibu Spika wa Bunge la Iraq Hassan Karim al-Kaabi ametoa wito kwa Saudi Arabia kukarabati Makaburi ya Baqii katika mji mtakatifu wa Madina.
Habari ID: 3472826    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/06/02

TEHRAN (IQNA) - Kumezinduliwa Kampeni ya Kimataifa ya kutaka misikiti miwili mitakatifu ya Makka na Madina isimamiwe kimataifa na nchi za Kiislamu.
Habari ID: 3472817    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/30

TEHRAN (IQNA) - Harakati ya Nujaba ya Iran imeilaani vikali televisheni Televisheni ya MBC ya Saudia ambayo imemvunjia heshima Shahidi Abu Mahdi al-Muhandis.
Habari ID: 3472771    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/16

TEHRAN (IQNA) –Nchini Yemen kumeripotiwa kesi kadhaa za ugonjwa wa COVID-19 au corona Jumatano huku Umoja wa Mataifa ukibainisha wasiwasi wake kuwa ugonjwa huo yamkini unaenea katika nchi hiyo bila kujulikana huku mamilioni wakikabiliwa na njaa na ukosefu wa huduma za afya.
Habari ID: 3472718    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/30