ashura - Ukurasa 6

IQNA

Ashura ni tukio ambalo imepita miaka takribani 1375 tokea kujiri kwake lakini si tu kuwa tukio hili la kihistoria linawavutia Waislamu bali pia wapenda uhuru kote duniani wamevutiwa na yaliyojiri katika jangwa la Karbala.
Habari ID: 3392955   Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/23

Idara ya waqfu iliyo chini ya Wizara ya Waqfu nchini Misri, imeamuru kufungwa msikiti wa Imamul-Hussein (as) mjini Cairo kuanzia jana Alkhamis hadi baada ya kesho Jumamosi ikiwa ni katika kuwazuia Waislamu wa Kishia kutekeleza marasimu za Taasua na Ashura.
Habari ID: 3392920   Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/23

Katika jitihada za kuleta umoja baina ya Waislamu wa madhehebu ya Shia, kumefanyika Majlisi za maombolezo Mwezi wa Muharram katika msikiti wa Masunni ambapo khatibu alikuwa ni mwanazuoni wa Kishia katika Kituo cha Kiislamu cha Dearborn, Michigan nchini Marekani.
Habari ID: 3391260   Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/21

Waislamu watano wa madhehebu ya Shia wameuawa nchini Saudi Arabia kufuatia hujuma ya kundi la kigaidi la Daesh au ISIS katika majlisi ya maombolezo ya siku 10 za Muharram.
Habari ID: 3386096   Tarehe ya kuchapishwa : 2015/10/17

Waislamu wa Kishia nchini Misri wamemwalika Sheikh Mkuu wa al-Azhar kuhudhuria shughuli ya maombolezo ya Ashura ya kukumbuka kuuawa shahidi Imam Hussein mjukuu wa Mtume Muhammad SAW.
Habari ID: 1465815   Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/31