iqna

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Msemaji wa serikali ya uwokovu wa kitaifa ya Yemen amekosoa kimya cha jamii ya kimataifa kwa jinai zinazofanywa na muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya watu wa Yemen na akasema, kuendelea kwa jinai hizo hakutakuwa na matokeo mengine isipokuwa wavamizi hao kufikwa na mwisho mbaya.
Habari ID: 3474722    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/25

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe wa hongera na pole kufuatia kuaga dunia kwa namna ya kufa shahidi Hasan Irlu, balozi mwanajihadi na mchapakazi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Yemen.
Habari ID: 3474710    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/23

TEHRAN (IQNA)- Kufa shahidi Hasan Irlu, balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Sana'a kumedhihirisha ukubwa wa jinai zinazofanywa na utawala wa Aal Saud nchini humo.
Habari ID: 3474709    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/22

Kamanda wa Kikosi cha Quds cha IRGC
TEHRAN (IQNA)- Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa, shahid Hasan Irlu (kwenye picha), balozi wa Iran nchini Yemen ambaye amefariki dunia kwa ugonjwa wa corona, alikuwa mtumishi wa wananchi madhulumu na wanamuqawama wa Yemen.
Habari ID: 3474701    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/21

TEHRAN (IQNA)- Mwanachama wa Idara ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarullah ya Yemen amedokeza kuwa, mkoa wa Ma'rib unakaribia kukombolewa kikamilifu kutoka mikononi mwa wavamizi wanaoongozwa na Saudi Arabia.
Habari ID: 3474658    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/09

TEHRAN (IQNA)- Msemaji wa Jeshi la Yemen amebainisha kuhusu "oparesheni ya Disemba Saba" na kueleza kuwa vikosi vya ulinzi vya Yemen vimetekeleza oparesheni ya kijeshi ya kipekee huko Riyadh, Jedddah, Taif, Jizan, Najran na Asir nchini Saudi Arabia.
Habari ID: 3474651    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/07

TEHRAN (IQNA)- Ndege za kivita za muungano vamizi wa Saudia zimedondosha mabomu katika wilaya ya Maqbanah mkoani Taiz nchini Yemen na kuua raia wasiopungua 16.
Habari ID: 3474638    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/04

TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Habari wa Lebanon George Kordahi amejiuzulu ili kupunguza mgogoro wa nchi yake na Saudi Arabia baada ya kauli yake ya kukosoa vita vya Saudia dhidi ya Yemen.
Habari ID: 3474634    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/12/03

TEHRAN (IQNA)- Shirika moja la kutetea haki za binadamu limesema mamia ya watoto wa Yemen wanafariki dunia ndani ya kila saa 24 kutokana na utapiamlo, huku muungano wa kivita unaoongozwa na Saudi Arabia ukiendelea kufanya mashambulizi na kuliwewekea mzingiro wa kila upande taifa hilo maskini la Kiarabu.
Habari ID: 3474584    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/21

TEHRAN (IQNA)- Kinara mmoja wa kundi la kigaidi la Al Qaeda amekiri kuwa kundi hilo linashirikiana kwa karibu na muungano vamizi wa Saudi Arabia katika vita dhidi ya Yemen.
Habari ID: 3474550    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/13

TEHRAN (IQNA)- Katika kulalamikia matamshi yaliyotolewa siku ya Ijumaa na George Kurdahi , Waziri wa Habari wa Lebanon aliyekosoa uvamizi wa Saudi Arabia na Imarati huko Yemen na kuutaja kuwa usio na maana, Saudia imemwita nyumbani balozi wake mjini Beirut na kumtaka balozi wa Lebanon pia aondoke nchini humo mara moja.
Habari ID: 3474498    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/11/01

TEHRAN (IQNA)-Saudi Arabia imemwita nyumbani balozi wake wa Lebanon na kumtaka balozi wa nchi hiyo pia aondoke mjini Riyadh, likiwa ni jibu kwa matamshi ya ukosoaji aliyotoa waziri wa habari wa Lebanon kuhusiana na uchokozi na uvamizi wa kijeshi uliofanywa na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudia dhidi ya Yemen.
Habari ID: 3474493    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/30

TEHRAN (IQNA)- Mamilioni ya watu wa Yemen wamejitokeza katika Maulidi ya Mtume Muhammad SAW y katika miji mbalimbali ya Yemen ukiwemo mji mkuu Sanaʽa.
Habari ID: 3474440    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/10/19

TEHRAN (IQNA)- Idadi kubwa ya wananchi wa Yemen Jumanne wamefanya maandamano makubwa katika mkoa wa Saada wa kaskazini wa nchi hiyo kwa mnasaba wa maadhimisho ya tarehe 21 Septemba, siku ya mapinduzi ya nchi hiyo.
Habari ID: 3474326    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/09/22

Kiongozi wa Ansarullah
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya Yemen amesema kuwa Saudi Arabia na Imarati ni nyenzo zinazotumiwa na Marekani.
Habari ID: 3474320    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/09/21

Kiongozi wa Ansarullah
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema Saudi Arabia, utawala wa Kizayuni wa Israel na Marekani ziko kwenye muungano mmoja.
Habari ID: 3474252    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/09/03

TEHRAN (IQNA)- Jopo la kisheria lililojumuisha mawakili walioko London ambao wanawakilisha waathirika wa mgogoro wa miaka mingi wa Yemen wametaka uchunguzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuhusu uhalifu wa kivita uliotekelezwa na muungano unaoongozwa na Saudi Arabia katika nchi hiyo masikini zaidi katika Bara Arabu.
Habari ID: 3474244    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/08/31

TEHRAN (IQNA)- Hali ya kibinadamu inayozidi kuwa mbaya nchini Yemen kutokana na vita vinavyoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo masikini ya Kiarabu na kusema kuwa, mtoto mmoja wa Yemen hupoteza maisha kila baada ya dakika 10.
Habari ID: 3474223    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/08/24

TEHRAN (IQNA)- Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen linasema linasubiri majibu chanya kutoka kwa Umoja wa Mataifa na mjumbe wake mpya wa Yemen, Hans Grundberg, kuhusu mpango uliopendekezwa na Harakati ya Ansarullah kwa ajili ya kusaidia kumaliza vita nchini Yemen.
Habari ID: 3474204    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/08/18

TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesisitiza kuwa hatua ya utawala wa Aal Saud ya kuzuia kufanyika ibada tukufu ya Hija kwa mwaka wa pili mfululizo kwa kisingizio cha corona ni kuivunjia heshima Nyumba Tukufu ya Allah.
Habari ID: 3474176    Tarehe ya kuchapishwa : 2021/08/10