IQNA

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran

Saudia inaweka vizuizi ili Wairani wasishiriki ibada ya Hija

22:02 - April 29, 2016
Habari ID: 3470278
Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema Saudia inaweka vizuizi ili Wairani wasishiriki katika ibada ya Hija ya mwaka huu.

Ayatullah Ahmad Khatami ameongeza kuwa Makkah na Madina ni miji muhimu ya ulimwengu wa Kiislamu na Aal-Saud hawana haki hata kidogo ya kuwazuia mahujaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kufika katika miji hiyo. Amesema kuwa, mahujaji wa Iran hawawezi kushiriki katika ibada hiyo chini ya anga ya kudhalilishwa au bila ya kudhaminiwa usalama wao. Ayatullah Ahmad Khatami aidha amekosoa vikali siasa za Saudia katika eneo la Mashariki ya Kati na kusema kuwa, Aal-Saud ni watekelezaji wa siasa za utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kwamba, wanaishambulia Yemen kwa lengo la kulinda maslahi ya Israel, kama ambavyo wanatenda jinai nchini Bahrain na kuyaunga mkono makundi ya kigaidi yanayofanya jinai kubwa dhidi ya binaadamu katika nchi za Syria na Iraq.

Kwingineko katika hotuba yake, Ayatullah Khatami amebaini kuwa,hatua ya Marekani ya kutwaa dola bilioni mbili mali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ni wizi wa wazi na ni kinyume cha sheria. Ayatullah Ahmad Khatami ameyasema hayo akijibu uamzi wa mahakama kuu ya Marekani wa kuzuia fedha hizo za Iran na kusisitiza kuwa, viongozi wa Iran kamwe hawatokubali mali ya taifa lao kuporwa, na kwamba, ni jambo lisilo na shaka kuwa, haki ya Iran itarejea nchini kutoka mikononi mwa Marekani.

3493092

captcha