Wizara hiyo imesema Uwanja wa Michezo wa Amani na Urafiki (SEF) eneo la Neo Faliro na Uwanja wa Olimpiki (OAKA) katika eneo la Maroussi ni maeneo ambayo yatakuwa wazi kutumiwa na Waislamu katika sherehe za kumalizika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani mapema mwezi Julai.
Makundi ambayo yanataka kutumia sehemu hizo yametakiwa kuwasilisha maombi kwa wasimamizi wa viwanja hivo kabla ya Juni 17.
Waislamu katika maeneo mengine ya Ugiriki wameshauriwa kuwasiliana na wakuu wa maeneo yao ili kujadli kuhusu sehemu za kusimamisha sala.
Waislamu Ugiriki kwa muda mrefu wamekuwa wakitaka ujwngwe msikiti mjini Athens ili kuweza kukidhi mahitaji ya jamii ya Waislamu wanaozidi kuongezeka.