Kwa mujibu wa matokeo ya awali chama cha PVV ( Party for Freedom) cha mwanasiasa mwenye
misimamo mikali ya kibaguzi na chuki dhidi ya Uislamu, Geert Wilders ,
kimepata viti 20 huku chama cha VVD
(Party for Freedom and Democracy) cha waziri mkuu wa sasa Mark Rutte
kikiwa kimepata viti 33 katika Bunge la Uholanzi lenye viti 150. Pamoja
na hayo chama chenye misimamo mikali kimepata viti vingi zaidi katika
uchaguzi huu kwani hapo kabla kilikuwa na vitu 12 huku chama cha VVD cha
waziri mkuu nacho kikionekana kupoteza umashuhuri kwani huko nyuma
kilikuwa na viti 41.
Katika matokeo mengine Vyama vya Christian Democrats na Democrats vimepata viti 19 kila kimoja
huku vyama vilivyosalia vya Kijani, Leba na Soshalisti vikinyakua viti
vilivyosalia. Asilimia 81 ya wapiga kura wanaripotiwa kushiriki katika
uchaguzi huo wa Jumatano na idadi hiyo imetajwa kuwa ya kihisotria.
Mwezi Disemba mahakama moja ya Uholanzi ilimpata wilders na hatia ya kuwatusi watu wenye asili ya Morocco na kuwabagua.
Kile kilichopelekea jina la
Wilders kupata umashuhuri katika miaka ya hivi karibuni ni hatua yake ya
kutengeneza filamu ya kuivunjia heshima Qur'an Tukufu ambacho ni kitabu cha
mbinguni cha Waislamu, filamu iliyoitwa jina la 'Fitina.'
Utengenezwaji wa
filamu hiyo uliibua malalamiko ya Waislamu duniani kote na hata kufunguliwa
mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo katika mahkama za Uholanzi.
Kufuatia ushindi wa Donald Trump mwenye chuki dhidi ya Uislamu katika
uchaguzi wa rais Marekani, wanasiasa wenye misimamo mikali ya mrengu wa kulia
kote Ulaya nao pia wamepata matumaini ya kunyakua madaraka. Hatahivyo matokea ya uchaguzi wa Uholanzi yameonysha kuwa watu wa Ulaya hawataki wanasiasa wenye misimamo mikali ya kufurutu ada.
Kwa kushindwa wanasiasa wenye misimamo mikali Uholanzi, kuna matumaini
pia kuwa wanasiasa wenye misimamo kama hiyo ya kufurutu ada nao pia
watashindwa Ujerumani na Ufaransa, nchi ambazo zinatarajia kufanya
chaguzi hivi karibuni.
3584709