IQNA

Misikiti ya Fiji kuruhusu wale tu waliopata chanjo ya corona

12:00 - October 02, 2021
Habari ID: 3474371
TEHRAN (IQNA)- Baraza Kuu la Waislamu Fiji limetangaza kuwa misikiti itafunguliwa tena nchini humo kuanzia Oktoba nne lakini watakaoruhusiwa ni wale tu waliopata chanjo kamili ya COVID-19 au corona.

Saiyad Hussain, Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Fiji amesema Waislamu wanaoingia misikitini  wanatakiwa kutumia aplikesheni ya simu za mkononi ya CareFiji.

Aidha amesema waumini wametakiwa wadumishe umbali wa mita mbili baina yao wakiwa msikitini na pia ni sharti kuvaa barakoa ili kuzuia kuenea corona.

Halikadhalika amesema wanaotaka kushiriki katika Sala ya Ijumaa wanapaswa kufika mapema msikitini ili kujisajili kwani hakuna atakayingia ndani ya msikiti bila kusajiliwa. Hussain amesema pia baada ya Sala waumini wanatakiwa kuondoka msikitini na wajiuzuie kujumuika makundi makundi.

Funguvisiwa la Fiji ni nchi iliyo kusini mwa Bahari ya Pasifiki na ina visiwa zaidi  300. Fiji ina idadi ya watu karibu milioni moja ambapo Waislamu ni karibu 60,000.

3475863

Kishikizo: fiji waislamu sala Corona
captcha