IQNA

Msikiti New Zealand unatumika kama kituo cha chanjo

21:42 - November 06, 2021
Habari ID: 3474524
TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Waislamu katika eneo la Manawatu New Zealand imeidhinisha msikiti wa eneo hilo kutumika kama eneo la kutoa chanjo ya COVID-19 kwa watu wote.

Nishar Ali, mweka hazina wa Msikiti wa Palmerston North, amesema wameamua kuinga mkono serikali ili ifikie lengo la chanjo kwa asilimia 90 ya watu wote nchini humo.

Amesema kuwepo zoezi hilo la chanjo ndani ya Msikiti kunawafanya Waislamu waafikie kuchanjwa huku walio na maswali wanauliza bila kuwa na wasiwasi hata kama hawaelewi Kiingereza.

Kuna Waislamu 1500 eneo la  Manawatu, na miongoni mwao ni wakimbizi 300 waliofika eneo hilo hivi karibuni na hivyo hawafahamu Kiingereza. Aidha katika msikiti huo wanawake Waislamu wanapata fursa ya kuchanjwa na wauguzi wanawake katika chumba tafauti na hivyo nukta hiyo imechangia kuongeza idadi ya wanaochanjwa.

3476361

captcha