Pamoja na kuwa misikiti ilifunguliwa tena nchini UAE Disemba mwaka jaana baada ya kufungwa kwa muda mrefu kutokana na janga la COVID-19 maeneo ya wanawake misikitini yalikuwa yangali yamefungwa.
Sasa kumbi za wanawake kusali zimefunguliwa kama ambavyo pia maeneo ya kutawadha na vyoo navyo pia vimefunguliwa. Hatahivyo waumini wametakuwa kuzingatia maelezo ya kiafya yaliyowekwa ili kuzuia kuenea COVID-19.
Daktari Saif Al Dhaheri Msemaji wa Mamlaka ya Kitaifa ya Kukabiliana na Maafa amesema misikiti yote itafungwa punde baada ya kila sala.