IQNA

Ifahamu Qur'ani Tukufu / 1

Kitabu Kilichotumwa na Mwenyezi Mungu

21:34 - June 06, 2023
Habari ID: 3477109
Tunapofikiria kitabu ni nini, maswali ya kwanza yanayokuja kichwani ni nani amekiandika na ni cha nani?

Qur'ani Tukufu ni kitabu kitukufu cha Waislamu ambacho kiliteremshwa kwa Mtukufu Mtume Muhammad (SAW) katika kipindi cha miaka 23. Msingi wa Qur'ani Tukufu ni matakwa ya Mwenyezi Mungu na hakuna yeyote, hata Mtukufu Mtume Muhammad  (SAW) amekuwa na haki ya kuibadilisha yaliyomo.

 Tunasoma katika Aya ya 44-46 ya Sura Al-Haqqa: “Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu, bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kuliaKisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!" 

Baadhi ya aya za Qur'ani Tukufu zina sifa maalum zinazoashiria kwamba Mwenyezi Mungu, Mwenyewe, ndiye anayezisema bila shaka yoyote:

  • Katika Aya ya 9 ya Surah Al-Hijr, Mwenyezi Mungu Anabainisha ni nani aliyekituma Kitabu: “Sisi wenyewe tumeiteremsha Qur’ani na Sisi ni Walinzi wake.
  • Katika baadhi ya matukio Wahy ulikuwa ni moja kwa moja, yaani, Mwenyezi Mungu aliiteremsha Qur'ani Tukufu moja kwa moja kwenye moyo wa Mtukufu Mtume Muhammad (SAW) na katika hali nyingine aliiteremsha kupitia Malaika Jibril (Gabriel). Mwenyezi Mungu Anasema katika Aya ya 97 ya Sura Al-Baqarah: “Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.” Aya hii inaonyesha Mungu anathibitisha uaminifu wa Jibril.
  • Qur'ani Tukufu iliteremshwa kwa moyo wa Mtukufu Mtume Muhammad (SAW). Mwenyezi Mungu anasema katika Aya ya 3-4 ya Surah An-Najm: “Hasemi kwa matamanio yake. Ni Aya zilizoteremshwa kwake.”

Nini maana ya Nuzul (kuteremsha) ya Qur'anI Tukufu ? Tunapozungumzia Nuzul, maana yake kuna sehemu ya juu ambayo kitu kinashuka. Qur'anI Tukufu imeteremshwa kutoka ulimwengu wa juu hadi kwenye ulimwengu huu lakini haimaanishi kuwa Mwenyezi Mungu ana nafasi mbinguni na ameiteremsha Qur'ani Tukufu kutoka mahali hapo bali inaonyesha hadhi ya juu ya Mwenyezi Mungu (Mwenyezi Mungu yuko kila mahali).

 

captcha