IQNA

Qari kijana wa Algeria akisoma aya za Surah Al-Baqarah (+Video)

IQNA- IQNA – Qari Kijana wa Algeria Abdul Aziz Sahim ameshiriki usomaji wake wa hivi majuzi wa aya kutoka kwenye Surah Al-Baqarah.

Ni qari mwenye talanta ambaye amepata kutambuliwa nchini Algeria. Kwa sasa Sheikh Sahim anaishi katika Umoja wa Falme za Kiarabu na ni Imamu wa sala katika  msikiti mmoja huko Ajman.

Mzaliwa wa M’sila, kaskazini mwa Algeria, Sheikh Sahim ameshinda mataji kadhaa katika mashindano ya kitaifa na kimataifa ya Qur'ani.

 

 


Ufuatao ni usomaji wake wa  Aya 285-286 za Surat Al-Baqarah:

Mtume ameamini yaliyo teremshwa kwake kutoka kwa Mola Mlezi wake, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na (Waumini) husema: Tumesikia na tumet'ii. Tunakutaka maghfira Mola Mlezi wetu! Na marejeo ni kwako. 285

Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyho. Faida ya iliyo yachuma ni yake, na khasara ya iliyo yachuma ni juu yake pia. (Ombeni:)Mola wetu Mlezi! Usituchukulie tukisahau au tukikosea. Mola wetu Mlezi! Usitubebeshe mzigo kama ulio wabebesha wale walio kuwa kabla yetu. Mola wetu Mlezi Usitutwike tusiyo yaweza, na utusamehe, na utughufirie, na uturehemu. Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tupe ushindi tuwashinde kaumu ya makafiri. 286

4194461

Kishikizo: algeria ، qari
Habari zinazohusiana