Makao Makuu ya Kimkakati ya Vyuo Vikuu vya Kiislamu (Hauza) ya teknolojia mahiri Smart Technologies yataandaa kongamano hilo maalum siku ya Alhamisi.
Mashirika na taasisi kadhaa kama vile Astan Quds Razavi, Makao Makuu ya Kimkakati ya Misikiti, Kituo cha Teknolojia ya Habari cha Hauza na Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (bunge la Iran) zitashirikiana katika kufanya hafla hiyo.
Wazungumzaji watajumuisha Hujjatul-Islam Ojaghnejad, msimamizi wa Msikiti wa Jamkaran, Reza Taqipour, mkuu wa Kamati ya Akili Mnemba ya Bunge, na Hujjatul-Islam Mohammad Mehdi Moslemifar, katibu wa Makao Makuu ya Mikakati ya Misikiti.
Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na juhudi za kuchunguza matumizi ya AI katika Hauza na vituo vya kidini.
Vituo vya Kiislamu nchini Iran vimekuwa vikikumbatia akili mnemba ili kusaidia katika uenezaji wa mafundisho ya kidini.
3491186